Thursday, December 16, 2010

Baraka Obama atangaza hali halisi ya Afghanistan.

Baraka Obama atangaza hali halisi ya Afghanistan. Washington, Amerika 15/12/2010 - Serikali na washiriki wake wanafanya kazi nzuri katika kuijengaAfghanistan na kuwaanda wananchi wa Afghanistan kuijenga nchi yao. Rais Baraka Obama, alisema "ingawaje hali ni ngumu lakini hii siyo kikwazo kwani, na nashukuru wale wote waliojitolea na kuendelea kujitolea pamoja na wapiganaji wetu ambao wanafanya kazi usiku na mchana ili kuijenga Aghanistan." Akiongezea rais alisema, "maendeleo yanaonekana na maendeleo haya ndiyo msingi mkubwa wa kuwafanya wananchi wa Afghanistan kuamini yakuwa kazi iliyo fanywa na jumuiya ya kimataifa ilikuwa ni kwa ajili ya wanachi wa Afghanistan." Baraka Obama, ameongea hayo ili kuwahakikishia wanachi wa Afghanistan ya kuwa Amerika ipo pamoja nao. Picha hapo juu anaonekana rais Baraka Obama, akiongea na waandishi wa habari ili kuzungumzia hali halisi ya Afghanistan na mipango ya kuisadia nchi hiyo kimaendeleo. Hatimaye mwanzilishi wa Wiki Leaks akubaliwa dhamana

London, Uingereza - 15/12/2010. Mahakama kuu jijini London imemwachia huru mwanzilishi wa Wiki Leaks baada ya mahakama ya mwanzo kukataa kumwachia huru kutokana na rufaa iliyo mtaka aendelee kukaa mahabusu.
Julian Assange 39 aliachiwa na kusema ya kuwa "anawashukuru wale wote walio changia kwa kiasi kikubwa hadi kuachiwa kwake na akasema ataendelea na kazi yake kama kawaida.
Assange anatakiwa Sweden kwa kosa la kufanya mapenzi ya kuchutukiza na moja ya wanamama wakati alipo kuwa nchini Sweden. Picha hapo juu anaonekana Julian Assange aliyeshikilia karatasi akitokea ndani ya mahakamani mara baada ya masharti ya dhamana kutimilizwa.
Serikali ya Amerika kuishitaki kampuni ya mafuta ya BP.
Washington, Amerika - 15/12/2010. Serikali ya Amerika imefungua kesi dhidi ya kampuni ya mafuta BP kutokana na uharibifu iliotokea baada ya mafuta machafu kuharibu mazingira katika pwani za Ghuba ya Mexico.
Mwanasheria mkuu wa Amerika, Erik Holder alisema, "uchafuzi wa mazingira ulio tokea ulisababishwa na BP kutofatilia sheria na kukamilisha maswala ya kiafya na usalama katika uchimbaji wa mafuta na tunaangalia ni kwa njia za kufanya ili kuhakikisha BP inawajibika kwa kuvunja sheria ya kuweka maji kuwa safi ( Clean Water Act )."
Uamuzi wa serikali ya Amerika kufuangua kesi dhidi ya BP, baada ya moja ya visima vyake kuvuja na kusambaza mafuta machafu katika Ghuba ya Mexico.
Picha hapo juu inaonyesha moja ya machafuko yaliyo sababishwa na mafuta machafu katika moja ya eneo la pwani ya Ghuba ya Mexico.
China na India kushirikiana kwa karibu zaidi.
New Dheli, India - 15/12/2010. Waziri mkuu wa China amefanya ziara nchini India ili kuendeleza uhusiano wa nchi hizo mbili.
Wen Jiabao amekutana na waziri mkuu wa Manmohan Singh na kujadili maswala mbalimbali ya ushirikiano kati ya nchi hizo mbili hasa katika kukuza biashara ambapo huenda ikafikiwa kiasi cha $ 100 Billion.
Ziara hiyo ya waziri mkuu wa China nchini India inatafsiliwa kuwa imekuja wakati muafaka kwani India ni nchi ambayo uchumi wake unakuwa kwa kasi. Waziri mkuu wa China, Wen Jiabao, akikagua gwaride lililo andaliwa wakati alipo wasili nchini India.
Hakimu, Duncan Ouseley alikataa maombi ya mwana sheria wa serikali ya Sweden ya kutaka Julian Assange aendelee kukaa mahabusu kwa madai ya kuwa "anaweza kukumbia."
Kuachiwa kwa Julian Assange, kumewezekana mara baada ya wadau wake kuchangisha kiasi cha US dollar zipatazo laki tatu na robo, chini ya uongozi wa watu mashuhuri kama Jemina Khan,Bianca Jagger, Ken LOach na John Pilger.
Picha hapo juu anaonekana Julian Assange akiingia mahakamani kusikiliza ombi la dhamana yake ambapo hapo mwanzo alikataliwa na mahakama ya mwanzo.

No comments: