Tuesday, December 21, 2010

Irak yapata serikali mpya.

India na Urussi kushirikiana kwa ukaribu zaidi. New Delhi, India - 21/12/2010. Serikali ya India na Urussi zimekubaliana kwa pamoja kushirikiana katika nyanja za kiusalama na kutiliana mikataba ya kibiashara uchumi na sayansi. Rais wa Urussi Dmirty Medvedev na waziri mkuu wa India Manmohan Singh walikubaliana mikataba hiyo wakati walipo kutana na kuzungumza ili kudumisha uhusiano zaidi. Ziara hiyo wa rais wa Urussi imekuja baada ya ziara za kufuatana za viongozi wa Uingereza, Amerika, China na Ufaransa kufanya ziarani nchini India ili kudumisha ushirikiano wakaribu. Picha hapo juu wanaonekana rais wa Urussi Dmirty Medvedev kushoto akipeana mkono na waziri mkuu wa India Manmouhan Singh mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo yao. Irak yapata serikali mpya.

Bagdad, Irak - 21/12/2010. Bunge la Iraki limekubaliana kwa pamoja kupitisha uteuzi wa waziri mkuu wa Irak na serikali yake na kutegua kitendawili cha kisiasa kilicho dumu zaid ya miezi tisa. Nouri al Maliki, ataiongoza serikali serikali ya Irak kwa kushirikisha makundi yote ya kisiasa ya Shia Sunn na Kurdi. Akiongea mara baada ya kupitishwa kwa serikali yake Nouri al Maliki alisema, serikali yake itajitahidi kwa kwa kila hali kuongoza wananchi wa Irak na ingawaje kwa sasa kunawakati mgumu ambao utasababisha baadhi ya mambo kuto fikiwa malengo kama ya livyo pangwa ili kuinua maisha ya wa Irak. Picha hapo juu anaonekana Nouri al Maliki kushoto akiwa na Ayad Allawi ambao hapo mwazo misimamo yao tofauti ilisababisha mvutano wa kisiasa kwa muda mrefu na kuleta wasiwasi mkubwa. Jeshi la umoja wa mataifa kuendelea kuwepo Ivory Coast.
Abidjan, Ivory Coast. 21/12/2010. Umoja wa Mataifa umekibaliana kwa pamoja kuendelea kuwepo kwa jeshi la Umoja la kulinda amani nchini Ivory Coast kwa kipindi zaidi cha miezi sita.
Jeshi hili lenye wapiganaji wapatao 10,000 litakuwa na majukumu mengine ya ziada, ikiwa ni kulinda wanchi na kupambana na mashambulizi ya aiana yoyote.
Uamuzi huo umechukuliwa baada ya rais wasasa Laurent Gbagbo, kulitaka jeshi hilo kutoka nchini humo mara muda wa makubaliana yaliyo wekwa utakapo kwisha.
Pia umija wa Ulaya na washiriki wake wamemwekea vikwazo rais Gbagbo na washirki wake wakaribu.
Msemaji wa Ikulu ya Amerika, Robert Gibbs alisema "inabidi Gbagbo aondoke madarakani mara moja."
Hata hivyo rais Laurent Gbagbo, bado anashikilia kiti cha urais huku akiungwa mkono na jeshi kwa kusaidiwa na wadau wake.
Picha hapo juu vinaonekana vifaru vya umoja wa mataifa vikiwa vimesimamishwa nje ya ofisi ya umoja wa mataifa iliyopo jiji Abidjan.

No comments: