Friday, December 24, 2010

Korea ya Kusini na Kaskazini wasiwasi wazidi kukuwa.

Makampuni ya Amerika yafanya biashara za kijamii na Iran.

New York, Amerika - 24/12/2010. Wizara ya biashara ya Amerika imetoa vibali kwa makampuni ili kufanya biashara nchini Iran kwa kipindi cha miaka kumi iliyo pita.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana vibali vipatavyo 10,000 vilitolewa kwa makampuni maalumu ili kufanya biashara za kusaidia jamii. Moja ya makampuni hayo ni Kraft Food, Pepsi na baadhi ya biashara za kibenki ambazo zilikuwa zinasaidia jamii katika maendeleo. Stuart Levey, msimamizi wa maswala ya vikwazo alisema " hii inafanyika kuhakikisha ya kuwa vikwazo visiathili watu hata wakafikia kukusa vyakula ambapo haitakuwa jambo la kiutu." Serikali ya Amerika iwekea Iran vikwazo ili nchi hiyo iweke wazi ukweli wake kuhusu mpango mzima wa mradi wake wa kinyuklia jambo ambalo Iran inalipinga na kukataa katakata kufanya hivyo. Picha hapo juu ni picha ya moja ya kampuni ambayo imewekeza kibiashara nchini Iran. Korea ya Kusini na Kaskazini wasiwasi wazidi kukuwa. Seoul, Korea ya Kusini 24/12/2010. Serikali ya Korea ya Kusini inaamini ya kuwa serikali ya Korea ya Kaskazini huenda ikafanya majaribio ya bomu la nyuklia mapema mwakani. Kutikana na ripoti kutoka wizara ya mabo ya nje ya Korea ya Kusini zinasema "majaribio hayo yatafanywa na Korea ya Kaskazini ikiwa ni njia moja wapo ya kukuza na kuangalia uwezo wa wake wa nguvu za Kinyuklia. Na majaribio hayo yatasababisha hali kuwa ya wasiwasi zaidi kati nchi hizo mbili." Korea ya Kaskazini ilifanya majaribio tofauti ya kinyuklia mwaka 2006 na 2009 kwa mujibu wa habari zinazoeleweka kimataifa, lakini Korea ya Kaskazini yanyewe haijawai kutamka kuhusu swala hilo. Picha hapo juu anaonekana mmoja wa mwanajeshi wa Korea ya Kaskazini akiwa katika moja ya vituo vilivyopo mpakani na Korea ya Kusini tayari kwa kazi ya ulinzi huku akiwa ameelekeza bundiki tayari. ECOWAS uenda ikatumia nguvu nchini Ivory Coast. Abidjan, Ivory Coast - 24/12/2010. Viongozi wa shirikisho la uchumi wa Afrika ya Magharibi (ECOWAS) wamemtaka rais wa sasa wa nchi hiyo kuachia madaraka mara moja. Viongozi wa shirikisho la ECOWAS walisema "ikiwa rais Gbagbo hatafanya hivyo basi itabidi nguvu zaidi itumike." Agizo hilo lilitolewa na viongozi wa ECOWAS lenye nchi wanachama 15 wakati walipo kutana jijini Abuja kujadili hali halisi ya Ivory Coast. Vurugu za kisiasa nchi Ivory Coast zilizidi mara baada ya matokeo ya uchaguzi wa rais kutangazwa na rais Laurant Gbagbo kudai ya kuwa ameshinda na huku mpinzani wake Alassane Ouattara akidai yeye ndiye aliye shida uchaguzi wa rais. Picha hapo juu anaonekana rais wa sasa wa Ivory Coast Laurent Gbagbo akiongea wakati wa kampeni zake za uchaguzi wa rias.

No comments: