Tuesday, December 14, 2010

Dunia ya mpoteza mtetezi wa amani.

Mahakama ya kubali maombi ya dhamana ya Julian Assange. London, Uingereza - 14/12/2010. Mahakama jijini London imekubali kumwachia kwa masharti mwanzilishi wa mtandao wa Wiki Leaks kwa dhamana ya dola za Kiamerika $ 317,400.

Julian Assange 39,ambaye anashitakiwa nchini Sweden kwa kosa la kufanya mapenzi ya kustukiza ambayo nimakosa nchini Sweden. Assange alijipeleka mwenyewe polisi mara ya karatasi ya kutaka kukamatwa kwake kutolewa na Interpol baada ya serikali ya Sweden kumfungulia mashitaka. Hata hivyo upo uwezekano wa serikali ya Sweden kupinga rufaaa hiyo. Picha hapo juu anaonekana Julian Assange ambaye anashukiwa na makosa ya kufanya mapenzi ya kushtukiza na moja ya mwanadada hivi karibuni nchini Sweden. Wanasheria wa Kenya wafikiria mara mbili mkataba wa Roma. Nairobi,Kenya - 14/12/2010. Kundi la wanasheria nchni Kenya wametishia kuandika barua kwa bunge la Kenya kufuta uanachama wake katika Mahakama ya Kimataifa (International Criminal Court-ICC). Kundi hilo la wanasheria walisema " tulitaka haki itendeke na mahakama ya kimataifa lakini haikuwa hivyo kutokana na uchunguzi wao. Na tunaangalia ni njia gani tutatumia kupitia bunge kujitoa katika matakaba wa Roma ( RomeStatute)." Mjadara huo umekuja baada ya ICC kusema inamajina sita ya watu waliohusika kuleta machafuko ya kisiasa kabla na baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika 2007. Machafuko hayo yalisababisha vifo vya watu zaidi ya 1500 na wengine 300,000 kuachwa bila makazi. Picha hapo juu anaonekana mmoja wa kijana akikimbia kuepusha maisha yake kutokana na machafuko yaliyo tokea kabla na baada ya uchaguzi nchini Kenya 2007 ambapo hali ya kiusalama ilikuwa imechafuka, kutisha kwa kilahali. Waziri mkuu wa Itali ashinda kura za maoni kwa mara nyingine. Roma, Itali - 14/12/2010. Waziri mkuu wa Itali ameshinda kura za maoni ambazo zilikuwa zimeitishwa zidi yake kutokana na baadhi ya wabunge na viongozi wa serikali kutokwa na imani naye. Silvio Berlusconi,ameshida kura hizo za maoni kwa kiasi cha uchache wa kura dhidi ya wale wanaopinga uongozi wake. Ushindi huo aliopata Berlusconi, siyo wa mara ya kwanza kwani alishida kura kama hiyo siku za nyuma. Hata hivyo wachambuzi wa mambo ya kisiasa wanasema Berlusconi atakuwa na wakati mgumu kuongoza serikali kutokana na upinzani mkubwa katika bunge na serikalini. Picha hapo juu anaonekana waziri mkuu wa Itali,Silvio Berlusconi akionyesha dole baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa kuwa ameshinda tena kura za maoni ambazo ziliitishwa na vyama vya upinzani hivi karibuni. Dunia ya mpoteza mtetezi wa amani.
Washington, Amerika - 14/12/2010. Mshauri mkuu wa serikali ya Amerika katika maswala na hali halisi ya nchi za Pakistan na Afghanistan amefariki dunia baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo kwa mara ya pili.
Habari kutoka Ikulu ya Amerika zimesema "Richard Holbrooke 69 alikuwa amelazwa katika hospital ya rufaa George Washington kwa ajili ya matibabu mara baada ya kupata matatizo ya moyo."
Rais wa Amerika Baraka Obama alisema " ameshutushwa na kifo cha Richard Holbrooke, na alikuwa mwananchi mwaminifu aliyependa nchi yake na kuitumikia kwa hali na mali, wanachi wa Amerika tomepoteza shujaa ambaye alikuwa mlinzi na mtetezi wa Amerika katika nyanja za kimataifa na kuhakikisha amani inapatikana kwa hali na mali."
Richard Holbrooke, alikuwa kinara katika kutetea na kuleta amani hasa katika nchi za Ulaya ya Mashariki zijulikanazo kama nchi za Balkans, pia kutumia mbinu zote kusimamisha vita vya Bosnia na alikuwa ni mmoja wa washauri wa rais Obama katika vita vinavyo endelea nchini Afghanista ili kujadili mbinu za kukabidhi madaraka kwa Waafghanistan.
Picha hapo juu anaonekana marehemu Richard Holbrooke, akiongea katika moja ya mikutano ya kimataifa enzi za uhai wake.

No comments: