Sunday, December 12, 2010

Waziri mkuu wa Itali kuwekwa kwenye boksi la maoni na wabunge.

Waziri mkuu wa Itali kuwekwa kenye boksi la maoni na wabunge. Roma, Itali - 12/12/2010. Wachunguzi wa serikali wameanza uchunguzi kufuatia kuwepo na habari ya kuwa waziri mkuu wa Itali ametoa milungula ili ashinde kura za maoni kuuhusu uongozi wake. Malalamiko hayo yalifunguliwa na kiongozi wa upinzani Antonia Di Puerto ambaye akikosoa uongozi wa waziri mkuu wa sasa Silvio Berluscon. Naye kiongozi mwingine wa chama cha upinzani Luigi De Magistris alisema "tumeona rushwa inatumika kati ya wabunge ili kumuunga mkono Berluscon." Hata hivyo Berluscon alisema "sidhani kama kutakuwa na wasaliti wengi na naimani serikali itashinda." Uamuzi wa kutaka kura za maoni zipigwe kumekuja kutokana na baadhi ya wabunge hasa wa upande wa upinzani kutokuwa na inami na waziri mkuu kutokana na habari za matukio ambayo yanamuhusisha moja kwa moja. Picha hapo juu ni picha waziri mkuu wa Itali, Silvio Berluscon ambaye serikali yake imekuwa na mvutano sana na vyama pinzani na kutaka kura za maoni zipigwe zidi ya uongozi wake.

Uchaguzi wa wabunge Misri waleta mvutano upya.
Kairo, Misri - 12/12/2010. Mamia ya watu wameaandamana kupinga matokeo ya uchaguzi wa wabunge kwa kudai ya kuwa haukuwa wea haki na kutaka mwanasheria mkuu kufuta matokeo.
Katika matokeo hayo chama tawala kinacho ongozwa na rais Housein Mubarak kimeshinda kwa kupata vitu vingi katika bunge. Naye msemaji wa mmoja wa chama cha upinzani George Ishak alisema "watu wanaandamana kupinga matokeo hayo na tutapinga kwa kufungua kesi ili kuonyesha ya kuwa uchaguzi haukuwa wa halali." Kufuatia matokeo hayo Mohamed ElBaradei aliyekuwa mkuu wa maswala ya Atomi amevitaka vyama vya upinzani kupinga kwa pamoja kushiriki katika uchaguzi wa urai uanaotarajiwa kufanyika mwaka ujao. Picha hapo juu wanaonekana polisi wa kuzuia ghasia wakiwa wanawazuia wananchi walioandamana mbele ya mahakama kuu kutoleta maafa na kuhakikisha usalama na amani unakuwepo. Japana kuweka mitambo ya kuzuia mashambulizi ya anga. Tokyo, Japan - 12/12/2010. Serikali ya Japan inajiandaa kuweka mitambo ya kuzuia
mashambulizi ya anga kutokana na kukua kwa mgogoro katika eneo zima la Asia Pasifiki. Habari zilizo patikana zinasema "mitambo aina ya Patriot Advavced Capabilty 3 itawekwa kuzuia mashambulizi ya anga pindipo kutatokea mashambulizi." Kitendo cha serikali ya Japan kuamua kuweka mitambo hiyo kinakuja kutokana na matukio ya Korea ya Kaskazini kuishambulia Korea ya Kusini hivi karibuni, jambo ambalo limezidi kuleta myumbo na mashaka katika eneo hilo la Asia Pasifiki. Picha hapo juu inaonekana moja ya mitambo ya kijeshi ambayo serikali ya Japan ina mpango wa kuiweka mitambo ya kivita ilikuzuia mashambulizi yoyote ya anga pindipo yatakapo fanyika. Wabunge wapinga malipo ya kiafya ya Septemba 11. Washington, Amerika 12/12/2010. Wabunge wa chama cha Republikan nchini Amerika wamepinga mswaada wa serikali kutaka kutoa malipo ya huduma za kiafya kwa wale wote walio athirika wakati wa mashambulizi ya Septemba 11/2001. Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema "kukataliwa kwa maswaada huo wa kuwasaidia malipo ya kiafya kutawaathiri pia wafanyakazi waliokuwa wanafanya kazi katika eneo hilo na wakazi wa vitingoji vya karibu na Ground Zero." Tangu tukio la Septemba 11/2001, wanasiasa wamekuwa wakipishana kimawazo kuhusu swala hili. Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya wafanyakazi wakiwa katika harakati za kusafisha mabaki ya majengo yaliyo bomoka, mara baada ya kulipuliwa na ndege zilizo tekwa nyara na magaidi.
Bomu lalipuka katikati ya jiji la Stockholm.
Stockholm, Sweden - 12/12/2010. Maofisa wa upelelezinchini Sweden wameanza rasmi kuchunguza tukio la bomu ambalo lililipuliwa katikati ya jiji la Stockholm jana.
Anders Thornberg ambaye ni afisa wa upelelezi alisema "tumeanza uchunguzi wa tukio hilo na tunalichukulia kama ni la kigaidi."
Katika mlipuko wa bomu hilo watu walijeruhiwa kutokana na mlipuko huo uliotokea jana wakati baadhi ya watu wakiwa mbioni kununua vitu kwa ajili ya kujianda na sherehe za Krismas
Hata hivyo shirika la habari la Sweden lilipata email iliyokuwa imeeleza kuwa huenda kukatokea tukio hilo kutokana na Sweden kujishirikisha katika vita vya Afghanistan na kitendo cha mchoraji mmoja raia wa Sweden kuchora picha ya kumkashifu Mtume Mohamed S.W.A.
Picha hapo juu wanaonekana wafanyakazi wa zima moto wakiwa wanazima moto uliotokana na mlipuko wa bomu kabla ya kuleta maafa makubwa.

No comments: