Friday, December 10, 2010

Ujerumani na Ufaransa zasema tutailinda sarafu ya Euro.

Ujeruman na Ufaransa zasema tutailinda sarafu ya Euro.

Freiburg, Ujerumani -10/12/2010. Kansela wa Ujerumani na rais wa Ufaransa wamekuta mjini Freiburg kujadili njia mbadala za kuimarisha sarafu ya Ulaya (EURO). Kansela Angela Markel na Nikolas Sarkozy walikutana na kuangalia kiundani njia ambazo zitaifanya sarafu ya Euro kuimarika zaidi hasa katika wakati uhu mgumu wa myumbo wa uchumi duniani. Viongozi hao kwapamoja walisema "tuta ilinda Eoro, kwani ni sarafu ya Euro ndiyo Ulaya yenyewe."

Kukutana kwa viongozi hao kunakuja kabla ya mkutan wa viongozi wa nchi wanachama wa jumuiya ya Ulaya kufanyika siku chache zijazo. Picha hapo juu anaonekana rais wa Ufaransa Nikolas Sarkozy kushoto akiongea huku Kansela Angela Markel akimsikiliza kwa makini sana na kutathmini nini hasa anaongea wakati walipo kutana hivi karibuni kujadili nini la kufanya ili sarafu ya Euro kuwa imara zaidi kimataifa. Zawadi ya Nobel yawekwa kwenye kiti cha mtarajiwa.

Oslo, Norway -10/12/2010. Sherehe za kumzawadia mshindi wa zawadi ya amani ya Nobel mwaka 2010 imefanyika jijini Oslo bila ya mzawadiwa kuwepo. Liu Xiaobo ambaye ni raia na mazaliwa wa China ndiye aliyekuwa mshindi wa zawadi ya amani ya mwaka 2010, lakini hakuweza kuudhulia sherehe hiyokwani anatunikia kifungo cha miaka 11 jela kwa kosa la uhani kwa mujibu wa sheria za China. Hata hivyo zawadi yake iliwekwa kwenye kiti ambacho alitarajiwa kukalia wakati wa kupokea zawadi hiyo. Thorbjoern Jagland ambaye ni mwenyekiti wa kamati hiyo ya kutoa zawadi alisema " Liu hajafanya kitu au jambo baya yeye ni mwanaharakati wa kutetea haki za binadamu." Msemaji wa serikali ya Chini Jiang Yu, alimesema "kutolewa kwa zawadi hiyo kwa Liu ni siasa iliyo shinikiza, ambayo ni zao la wakati wa vita vita vya baridi, na hivyo China haitakukubali kuingiliwa katika maamuzi yake." Picha hapo juu wanaonekana wageni waalikwa wakiangalia picha ya Liu Xiaobo aliye tunikiwa zawadi ya amani ya Nobel 2010 lakini hauwepo kwenye sherehe hizo na zawadi yake kuwekwa kwenye kiti alicho tarajiwa kukikalia.

No comments: