Wednesday, December 15, 2010

Ghana kuanza kuzalisha mafuta.

Irak yaondolewa vikwazo na Umoja wa Mataifa. New York, Amerika - 15/12/2010.Kamati ya usalama ya umoja wa Mataifa imeiondolea vikwaza nchi ya Irak iliyo kuwa imeviweka kwa muda wa zaidi ya miaka 19. Akiongea katika mjadala wa kutaka kuiondolea vikwazo Irak, makamu wa rais wa Amerika Joe Biden alisema "Irak inahitaji kuwa katika kiwango cha kimataifa kwa kujitegemea yenyewe na demokrasi ndiyo msingi mkubwa ambo utifanya nchi hiyo imeze kuendelea na Wairak wameonyesha uwezo huo. Pia ni muhimu kwa Irak kuwa na uhusiano mzuri na majirani zake kwani bado Wairak wanamthian mkubwa mbeleni." Katika kikao hicho, kamati ya usalama iliondo vikwazo vyote ilivyoviweka kwa Irak na kupitisha mswada ambao umeiruhusu Irak kuweza kujenga mtambo wa nyuklia kwa matumizi ya kawaida. Vikwazo kwa Irak viliwekwa mwaka 1991 na umoja wa Mataifa mara baada ya Irak kuivamia Kuwait mwaka 1990 enzi ya utawala wa rais Saddam Huissen ambaye alitolewa madarakani na serikali ya Amerika mwaka 2003 baada ya kushukiwa kuwa na siraha za kuangamiza jamii. Ghana kuanza kuzalisha mafuta. Akrah, Ghana - 15/12/2010.Wananchi wa Ghana kwa mara ya kwanza wameungana na nchi nyingine dunia katika kuzalisha mafuta kutoka kwenye Ghuba ya Guinea. Akifungua kuanza kwa uzalishaji huo rais wa Ghana John Atta Mills alisema "kuzalishwa kwa mafuta hayo ni baraka na siyo laaana kwa wananchi wa Ghana, na mafuta yatakayo patikana yataisaidia Ghana kuinua uchumi wake zaidi kulio ilivyo sasa." Kiasi cha mapipa 55.000 yanatarajiwa kuzalishwa kwa siku. Eneo hilo liligunduliwa kuwa linamafuta miaka mitatu iliyo pita na kampuni moja ya Uingreza Tullow Oil PLC. Picha hapo juu ni ya ramani ya nchi ya Ghana ikiwa imefunikwa na rangi za bendera ya nchi hiyo ambayo kwa sasa inatambulika rasmi kuwa mzalishaji wa mafuta na kujiungana na nchi nyingine zilizopo katika bara la Afrika. Wanasiasa maarufu Kenya wahusishwa katika machafuko ya 2007

Nairobi, Kenya - 15/12/2010. Mwanasheria mkuu wa mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai ametangaza rasmi majina ya watu walioshukiwa kuhusika na machafuko wakati na kabla uchaguzi mkuu uliofanyika 2007.
Moreno Ocampo, alitangaza majina hayo "Uhuru Kenyatta ambaye ni waziri wa fedha, William Ruto, Fransis Muthaura, Joshua Arap Sango mwandishi wa habari, Henry Kosgey na mkuu wa polisi wa zamani Mohamed Hussein."
Akiongea mara baada ya kumaliza kutaja majina hayo, Moreno alisema watu hawa washukiwa hawa bado hawana makosa mpaka hapo mahakama itakapo wakuta na hatia.
Uamuzi huo wa mahakama ya kimataifa kuingilia kati swala hilo la kutafuta ukweli ni watu gani walikuwa vinara wa kuongoza machafuko ulikuja kutokana na serikali ya Kenya kuchukua muda kuwatambua watu hawa waliotajwa.
Picha hapo juu ni ya bendera ya Kenya nchi ambayo ilikuwa na machafuko makubwa ya kihistoria katika nchi hiyo tangu kupata uhuru kutokana na mvutano wa kisiasa na itikadi zilizopo kati ya wananchi wake.

No comments: