Monday, April 25, 2011

Taliban wavunja jela na kutoroka.

Gaidi akamatwa nchi Venezuela.
Caracas, Venezuela - 25/04/2011. Maafisa wa usalama serikali ya Venezuela wamemkamata gaidi ambaye ameshukiwa kutaka kuhusika na kitendo cha kigaidi.
Kwa mujibu wa habari kutoka serikali ya Venezuela zinasema "gaidi huyo Joaquin Perez Becerra alikamatwa siku jumamosi baada serikali ya Kolombia kuwasiliana na serikali ya kuwa gidi huyo atapitia nchini"
Kukamatwa huko kwa Perez kuna kumekuja baada ya Interpol kutoa hati ya kukumatwa kwake wakati akitokea nchini German.
Huusiano wa serikali ya Venezuela na Kolombia umekuja baaada ya nchi hizo kukubaliana kushirikiana kiusalama baada ya rais mpya wa Kolombia Juan Manuel Santos kukutana na rais wa Venezuela Hugo Chavez na kuongea kumaliza uhasama kati ya nchi hizo mbili.
Taliban wavunja jela na kutoroka.
Kandahar, Afghanistan 25/04/2011. Zaidi ya wafungwa mianne wametoroka kutoka katika jela moja ambayo wengi wa wafungwa hao walikuwa wapiganaji wa kundi la Taliban.
Wafungwa hao ambao wametoroka kupitia shimo walio lichimba kwa urefu chini ya ardhi hadi kutoke nje gereza bila watu wausalama kutambua.
Msemaji wa Zabuillah Mujahed alisema " shimo hilo lilichimbwa kwa muda wa miezi mitano na walichukua masaa manne na nusu kutoka ndani ya jela hiyo.
NATO, alitibitisha habari hizi kwa kusema " tuna habari ya kuwa wametoraka kupitia shimo ambalo walilichimba kwa umbali wa zaidi ya mita 320.
Naye msemaji wa serikali ya Afghanistan, Waheed Omer kutoroka kwa wafungwa hao siyo picha nzuri kwa serikali , na tutahakikisha tunawakama wote waliotoroka."
Hii itakuwa ni mara ya pili wa wafungwa kutoka toka jela, baaada ya tukio kama hili mwaka 2008 ambapo wafungwa wapatao 1,000 walitoroka.
Makazi ya Muammar Gaddafi yashambuliwa.
Tripoli, Libya 25/04/2011.Ndege za jeshi la NATO limeshambulia makazi ya rais wa Libya ambaye majeshi yake yanapambana na majeshi ya upinzani yanayo ungwa mkono na Ufaransa, Uingereza na jumuia ya NATO.
Msemaji wa serikali Mussa Ibrahim amesema " ndege za jeshi la NATO lilishambulia makazi hayo kwa nia ya kutaka kumua rais wa sasa Muammar Gaddafi, ambaye nchi wanachama wa NATO zinataka atoke madaraka kwa kutumia nguvu za kijeshi jambo ambalo linaonyesha nini nia ya NATO."
Katika mashambulizi hayo, baadhi ya raia na wanajeshi waliokuwepo kwenye eneo hilo wanjeruhiwa vibaya na kuharibu kwa kiasi kikubwa majengo ya eneo hilo lililopo Ba el Azizia.

No comments: