Friday, April 15, 2011

Obama,Sarkoz na Kameron tutahakikisha Gaddafi anang'oka.

Obama, Sarkoz na Kameron tutahakikisha Gaddafi anang'oka.

London, Uingereza 15/04/2011. Viongozi wa Uingereza, Ufaransa na Amerika wamekubaliana kwa pamoja kuundeleza mapambano dhidi ya kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi.
Nikolas Sarkozi rais wa Ufaransa, waziri mkuu wa Uingereza David Kameon na rais wa Amerika Baraka Obama, kwa pamoja wamekubaliana kuhakikisha kiongozi wa Muammar Gaddafi anatoka madarakani.
Viongozi hao walitoa waraka wao wa pamoja na kusisitiza "sheria ya muswada ya kamati ya usalama ya umoja wa mataifa ya 1973, inataka jumuia ya kimataifa kulinda usalama wa raia na razima waitekeleze."
Waraka huo uliongezea " NATO na washiriki wake wataendelea na jukumu lao la kulinda raia na kuhakikisha Kanali Muammar Gaddafi anatoka na kuwapa uhuru wa na nchi wa Libya kujitawala wenyewe.
Hata hivyo baada ya waraka huo kutoka, kiongozi wa Libya alionoekana katika mitaa ya Tripoli akiwaslimia wanchi na wadau wanao muunga mkono, na huku mwanae wa kike Aisha Gaddafi aliwahutubia watu waliokuja Bab al Azizyah kuadhimisha miaka 25 tangu Amerika ilipo vamia Libya na kusema baba yake hataachia madaraka kwa kulazimishwa wala vitisho vya nchi za Magharibi na washirika wake.

No comments: