Wednesday, April 13, 2011

Viongozi wakutana Katar kutathmin hali ya Walibya.

Nchi zinazo ongoza kukua kwa uchumi dunia zakutana nchini China. Hainan, China 13/04/2011. Viongozi wa serikali na mabenk wamekutana nchi China ili kuangalia kiundani njia bora ya kuimarisha sekta ya bishara ya kifedha na uchumi.

Li Wuwei, makamu wa mwenyekiti na mshauri wa mambo ya kisiasa alisema, " nchi wanachama zimejitahidi na kushirikiana katika kuinua hali ya kiuchumi baada ya ya myumbo wa kiuchumi kutokea na zitaendele kufanya hivyo hasa katia nchi zinazohitaji kuinuka kiuchumi ili ziweze kukidhi mahitaji ya jamii zao."
Mkutano huo unaojulikana kama BRICS unajumuisha nchi za Brazil, Urussi, China na Afrika ya kusini nchi ambazo zinaongoza katika kukua kwa uchumi kwa haraka zaidi.
Rais wa zamani wa Misri na watoto wake wawekwa chini ya ulinzi wa polisi.
Kairo, Misri 13/04/2011. Rais wa zamani wa Misri amewekwa kizuizini pamoja ya watoto wake wawili wa kiume, ilikuwezesha uchunguzi zidi ya kesi inayo wakabili ya rushwa na unyanyasaji.
Kwa mujibi wa wakili wa serikali alisema " Hosni Mubaraka na watoto zake Gamal na Alaa watakuwa kuzuizini kwa muda wa siku15 wakati uchunguzi unaendelea zidi yao."
Hosni Mubaraka 82, ambaye ametawala Misri kwa miaka zaidi ya miongo mitatu alitolewa madarakani na maandamano ya watu waliotaka aachie madaraka mapema mwanzoni mwa mwaka huu..
Habaria zinasema rais Hosni Mubaraka anamatatizo ya moyo na hivi sasa yupo hspitali amelazwa kwa uchunguzi zaidi wakati watoto wake wako chini ya ulinzi wa polisi.
Viongozi wakutana Katar kutathmini hali ya Walibya.
Doha,Katar - 13/04/2011. Viongozi wa kundi la upinzani linalo pingana na serikali ya Libya wamekutana na viongoziwa nchi tofauti nchi Katar ili kujadili hali halisi ya mapambano yanayo endelea ili kung'oa madarakani kiongozi wa Libya MuammarGaddafi.
Akiongea mbele ya viongozi walioudhuria mkutano huo waziri wa mambo ya nchi za nje wa Uingereza William Hague amesema, "nilazima tuhakikishe tunafanya kila njia ili tunasaidia kundi la upinzani ili kuliwezesha kuimarisha demokrasi nakuhakikisha Muammara Gaddafi anakubaliana na matwakwa ya wanchi wa Libya."
Msemaji wa kundi la upinzani linalo mpinga serikaliya Mahmud Shamman alisema, " tungependa tutambulike kama wawakilishi wa serikali mpya ya Libya ambao tupo kwa ajili ya kuijenga Libya kwa kila Mlibya."
Mkutano wa huu umefanyika ili kuangalia ni kwa kiasigani jumuiya ya kimataifa itaweza kuisaidia Libya.

No comments: