Thursday, April 7, 2011

Mahakama ya Hague yaanza kesi za machafuko ya Kenya.

Mahakama ya Hague yaanza kusikiliza kesi za machafuko ya Kenya.

Hague, Netherland -07/04/2011. Viongozi wa siasa kutoka nchini Kenya wamefikishwa mahakamani kufuatia machafuko yaliyo tokea wakati na kabla uchaguzi.
William Ruto,Henry Kosges ambao walikuwa mawaziri na mtangazaji Joshua Arao Sang wanashita kwa kuchochea machafuko ya kikabila yaliyopo nchini Kenya.
Hata hivyo bado kuna watuhuniwa wengine wanatarajiwa kufikishwa mahakani kujibu mashitaka kama haya.
Uchaguzi wa urais wa mwaka 2007 nchini Kenya ulileta machafuko ya kisiasa na hata kupelekea kumwagika kwa damu na watu kupoteza maisha yao.
Japan yakumbwa na tetemeko la ardhi jingine.
Tokyo, Japan -07/04/2011. Tetemeo kubwa la ardhi limeikumba tena Japan baada ya tetemeko la kwanza ambalo limeleta maafa makubwa.
Tetemeko hili lililo tokea kaskazini mwa Japan, limepelekea jamii nzima ya maeneo imetakiwa kuondoka kwani kunawasiwasi tsunami kutokea.
Wataalamu wa mambo ya kiyasansi ya ardhi na hali ya hewa wamesema "tete hilo limekuwa na nguvu za uwezo wa 7.1 magnitude."
Hata hivyo mpaka sasa hakuna habari zaidi kimaafa na watu kupoteza maisha.

1 comment:

yak kate said...

hello, i am young pretty single girl,i am caring,loving,affectionate,compassionate and always ready for a new adventure.contact me by email : yakkate@yahoo.com one love, kate.