Friday, April 22, 2011

Ndege aina ya Drone kuanza kutumika nchini Libya.

Umoja wa Afrika waondolea vikwazo Ivory Coast.
Adis Abeba, Ethiopia -22/04/2011. Umoja wa Afrika umeondoa vikwazo amba
yo vilikuwa vimewekwa zidi ya nchi ya Ivory Coast.
Akiongea kuondolewa kwa vikwazo hivyo, mwenyekiti wa kamati ya amani ya Umoja wa Afrika alisema " tunapenda serikali iliyo chukua madaraka ihakikishe yakuwa ina imarisha usalama, haki na amani kwa watu wote katika misingi ya kidemokrasia na kuanzisha mpango mzima wa watu kusameheana."
Uamuzi huo umekuja baada ya aliye kuwa rais wa nchi hiyo Laurent Gbagbo, kutolewa madarakani kwa nguvu na jeshi la Alassane Ouattara kwa kusaidiwa na jeshi la Ufaransa.
Wapinzani hao katika kiti kugombea kiti cha urais Laurent Gbagbo na Alassane Ouattara walianza kuvutana kisiasa baada ya matokeo ya uchaguzi kutolewa n a huku kila mmoja kudai ndiye aliye ibuka mshindi.
Ndege aina ya Drone kuanza kutumiwa nchi Libya.
Benghazi, Libya 22/04/2011. Aliyekuwa mgombea wa kiti cha urais na ambaye pia ni mbuge wa chama cha Republikan cha Amerika amewasili nchini Libya.
John McCain, amewasili nchini Libya ili kuongea na viongozi wa upinzani ambao wanapingana na serikali ya Libya inayo ongozwa na Kanali Muammar Gaddafi.
Akijibu swali nini nia ya madhumuni ya ziara yake nchini humo, McCain alisema " nimekuja ili kuangalia hali halisi kutokana na matukio yanayo endelea."
Kuwasili huko kwa McCain kumekuja baada ya rais wa Amerika Baraka Obama kuruhusu matumizi ya ndege Drones ambazo zinatumia nguvu za mtandao katika kufanya mashambulizi zitumike katika vita zidi ya serikali ya Libya.

No comments: