Monday, April 11, 2011

Iceland yasumbua vichwa vya wafadhili wake.

Iceland yasumbua vichwa vya wafadhili wake.

Hague, Netherland - 11/04/2011. Serikali ya Uingereza na serikali ya Netherland zimeishitaki serikali ya Iceland baada ya kutoke mgogoro wa kulipa deni.
Uamuzi huo wa serikali hizo kuishitaki Iceland limekuja baada ya wanchi wa Iceland kupinga kitendo cha serikali yao kulipa deni la pesa ambazo ziliazimwa kwa Iceland ili kusaidi serikali ya nchi hiyo baada ya myumbo wa Mabenki nchini humo.
Hata hivyo msemaji wa serikali ya Iceland alisema " serikali ya Iceland haina wasiwasi n aitalipa dei hilo, hata kama wanachi hawapendelei kitendo hicho."
Serikali ya Iceland ilipewa pesa na serikali za Uingereza na Netherland ili kuimarisha mabenki yake baada ya kutokea kwa myumbo wa kipesa na kutishia uchumi wa Iceland.

No comments: