Julian Assange aanzisha kipindi kwenye Luninga -TV ya Kirusi RT News.
Moscow, Urussi - 17/04/2012. Mwanzilishi wa mtandao wa WikiLeaks ameanzisha kipindi cha mazungumzo katika luninga TV kupitia luninga TV ya kitaifa ya Urussi.
Julian Assange ambaye yupo chini ya ulinzi kwa kufungiwa kutokutembea huru, katika ufunguzi wa kipindi chake cha mazungumzo ya Luninga kwa mara ya kwanza amefanya mazungumzo na kiongozi wa kundi la Hezbollah Said Hassan Nasrallah ambaye hajawahi kufanya mahojiano na vyombo vya habari kwa muda mrefu.
Kipindi hicho kitajulikana kama The World Tomorrow, ambapo wageni mbali mbali wataalikwa kufanya mazunguzo naye.
Akiongea kabla ya kuanza kipindi hicho Julian Assange alisema "kwa kuwa na kifungo cha nyumbani, itakuwa vizuri kuweza kuongea na watu tofauti na kujifunza toka kwao."
Julian Assange yupo chini ya ulinzi kwa muda wa siku 500 sasa baada ya kesi iliyofunguliwa zidi yake ya kuhusika katika kubaka mwanadada mmoja wakati alipo kuwepo nchini Swiiden, jambo ambalo Assange anakanusha yakuwa hakumbaka mwana dada huyo.
Baraka Obama aongoza katika kura za maoni zidi ya Mitt Romney.
Washington, Marekani - 17/04/2012. Wachunguzi wa mambo ya kisiasa nchini Marekani wametoa matokeo ya utafiti wa kura za maoni wa ugombea urais ambao unaonyesha rais wa sasa Baraka Obama anaongoza.
Kwa mujibu wa kura hizo za maoni, "Baraka Obama wa chama cha Demokratic anaongoza kwa 52% na mpinzani wake Mitt Romney wa chama cha Republikan kupata kura za maoni 43%." na wanacha wa chama Demokratik kudai ya kuwa Baraka Obama ndiye kiongozi anayefaa kuingoza tena Marekani.
Matokeo hayo yamekuja baada ya mgombea mwenza wa chama cha Republikan Rick Santorum kujitoa katika kinyang'anyiro cha kugombe kiti cha urais wa Mareakani na kumwachia nafasi mgombea pekee kupitia chama hicho Mitt Romney.
Pilika za kutaka kuwania kiti cha urais nchini Marekani zimeshaaanza kwa mwendo wa gia namba moja tayari kwa kila mgombea kujipanga wakati wa safari hiyo ndefu ya kutaka kuingia Ikulu ya Marekani.
Iran yadai Saudi Arabia haina uwezo wa kuziba pengo la mafuta.
Waziri Rostam Qaesem alisema " Saudia Arabia inaweza kutoa mafuta hayo kwa muda mfupi, lakini kwa kipindi kirefu hawataweza na matokeo ya ahaadi hiyo yataleta mashaka katika dunia."
Maelezo hayo ya Iran yamekuja baada ya serikali ya Saudi Arabia kuhaidi yakuwa inauwezo wa kuziba pengo la mafuta litakalo tokea baada ya Iran kuwekewa vikwazo kwa kuzalisha mafuta zaidi.
Iran imewekea vikwazo vya uuzaji wa mafuta, benki na biashara katika masoko ya nchi za Ulaya Magharibi na Marekani, baada ya Iran kuendelea na mpango wake wa mradi wa kinyukilia.
No comments:
Post a Comment