Tuesday, April 10, 2012

Serikali ya mpito ya Libya yapingana na mahakama ya Kimataifa.

Zintan, Libya - 10/04/2012. Serikali ya Libya imeitaka mahama ya kimataifa inayo shughurikia makosa ya jinai na kutetea haki za binadamu kutoa muda ili kuweza kuaanda kesi ya mtoto aliyekuwa mtoto wa rais wa Libya Muammar Gaddafi.
Serikali ya mpito ya Libya iliomba kwa kusema " Libya haitampeleka Saif al Islam Gaddafi nchi Uhollanzi kwani serikali ya Libya inauwezo wa kuendesha kesi zidi yake."
Seif al Islam Gaddafi ambaye alikamatwa baada ya baba yake Muammar Gaddafi kuangushwa kutoka katika kiti cha urais na kuwawa, anashutumiwa kwa kuhusika katika kukiua haki za binadamu wakati wa utawala wa baba yake.

Mozambique na Ureno zazungumzia utata wa bwawa la Cahora Bassa.


Maputo, Mozambique - 10/04/2012. Serikali ya Mozambique na Ureno zimekubaliana kudumisha ushirikiano wa karibu zaidi ili kweza kushirikiana kwa kila nyanja za kiuchumi na biashara.
Makubaliano hayo serikali ya Mozambique na Ureno yamekuja baada ya ziara ya waziri mkuu wa Ureno  Pedro Passos kufanya ziara nchini  Mozambique  na kubaliana kuangalia upya ni kwa jinsi gani mzozo wa bwawa la Cahora Bassa ambao ulikuwa haujatafutiwa ufumbuzi.
Mozambique ilikuwa koloni la Ureno kabla ya kupata uhuru mwaka 1975 chini ya chama cha FRELIMO.
na uhusiano kati ya nchi hizombili kupungua kwa muda mrefu.

Mtuhumiwa wa mauaji ya Norway adaiwa ni mzima wa akili.


Oslo, Norway - 10/04/2012. Wachunguzi wa afya ya akili  walio mfanyia  mtu aliye husika katika  mauaji ya kutisha yaliyo tokea nchini Norway mwaka 2011/ Julai/22 wametoa majibu kuhusu hali ya akili ya mshutumiwa huyo .
Anders Behring Breivik 33 ambaye aliwauwaa watu 77 na kutega mabomu ambayo yalileta maafa makubwa ameripotiwa na wachunguzi wa afya ya akili yakuwa akili yake haipo katika hali ya kufanya unyama na ni mzima.
Majibu kuhusu ali ya kiafya ya kiakili juu ya Breivek yamekuja baada ya uchunguzi zaidi kufanywa kuhusu afya yake.
Awali mtuhumiwa Anders Behring Breivik alidhaniwa ya kuwa anamatatizo ya akili, jambo ambalo lilifany wakili kufikilia ni kwa jinsi gani watashughurikia kesi ya muaaji huyo.

Iran yadai kuwakamata majasusi waliotaka kufanya mashambulizi hivi karibuni.


Tehran, Iran - 10/04/2012. Wizara ya usalama ya Iran imetangaza yakuwa imewakamata watu kadhaa na kufanikiwa kuvunja nguvu za majasusi ambao walikuwa wamepanga kufanya mashambulizi nchini humo hivo karibuni.
Kwa kujibu wa habari zinasema " baada ya kukamatwa kwa watu hao, ushahidi umeonekana ya kuwa kuna nchi za Ulaya Magharibi  Marekani na washiriki wake wanahuzika katika ujasusi huo.
Idadi ya siraha na mabomu na mitambo mingine ya kijeshi ilikamatwa wakati baada ya wapelelezi wa Iran kupata uhakika kamili."
Kufuatia kukamatwa kwa watu hao, serikali ya Iran imedai ya kuwa habari nyingine zitafuatia hivi karibuni ili kuthibitisha mpango huo wa majasusi.ulikuwa ni wa kweli.
Iran imekuwa inavutana na nchi za Magharibi, hasa katika swala  la utengenezaji nguvu za kinyuklia, ambapo Iran inadai ni haki yake kuwa na uwezo wa kutengeneza nguvu za nyuklia.

No comments: