Friday, April 27, 2012

Rais wa zamani wa Liberia akutwa na hatia.

Wake wa Osama bin Laden warudishwa Saudi Arabia.


Abbottabad, Pakistan - 27/04/2012. Wanawake waliokuwa wake wa kiongozi wa kundi la Al Qaeda, wamerudishwa nchi Saud Arabia.
Kwa mujibu wa habari kutoka serikalini zinasema " wake hao wawili wa Osama Bin Laden wamerudishwa  nchini Saud Arabia pamoja na watoto 11."
Wake hao watatu wa Osama Bin Laden walikamatwa na kuwekwa kizuizini mara baada ya mume wao kuuwawa na jeshi la Marekani mwaka 2011 mwezi May.
 
Rais wa zamani wa Liberia akutwa na hatia.

Hague, Uhollanzi - 27/04/2012. Aliyekuwa rais wa Liberia  amekutwa na hatia ya kukiuka haki za binadamu wakati akiwa kiongozi  wa nchi kwa kusadia kundi la lililo sababisha mauaji, ubakaji na unyanyaswaji nchi Sierra Leone kati ya mwaka 1996-2002.
Charles Tylor alikutwa na hatia hiyo kwa kulisaidia kundi la Revolutionary United Front (RUF) and Army Revelutionary Council (AFRC).
Hata hivyo Charles Tylor amekanusha kuhusika na vitendo hivyo.
Kufuatia kukutwa na hatia hiyo, hukumu juu ya Charles Tylor itatolewa hivyi karibuni na anatarajiwa kutumikia kifungo nchi Uingereza.