Thursday, April 5, 2012

Rais wa Malawi alazwa hospitali.

Raia wa Urussi haukumiwa miaka 25 jela nchini Marekani.

New York, Marekani - 05/04/2012. Jaji wa mahakama katika jiji la New York amemuhukumu kwenda jela miaka 25 raia wa Urussi ambaye alikuwa mfanya biashara wa kuuza siraha.
Voktor Bout 44 ambaye alipiga ukelele kwa kusema " huu ni uongo" alikutwa na hatia ya kuhusika na njama za kuhatarisha maisha ya Wamarekani na kwa kutaka kuuza siraha kwa magaidi.
Pia inaaminika mtuhumiwa Viktor Bout, alihusika katika kuuza siraha nchi za Rwanda, Angola na Congo.
Hata hivyo upande wa utetezi wa Viktor Bout ulidai yakuwa mteja wao alikuwa akiuza ndege mbili za mizigo zanye thamani ya $5million.

Pakistani yataka ushahidi kamili kutoka na madai ya  Marekani.

Islamabad, Pakistan - 05/04/2012. Serikali ya Pakistani imeitaka serikali ya Marekani kutoa ushahidi kamili wa madai yakuwa raia wa Pakistan alihusika katika milipuko iliyotiokea nchini India 2008.
Habari kutoka ofisi ya mambo ya nje ya Pakistani zinasema "tungependa tupate ushahidi wa kutosha ili tuanze kufuata sheria badala ya kuongelea kwenye mitandao na njia tofauti.
Mohammad Saeed alisema " nipo naishi maisha yangu ya kila siku bila shida na kama kuna mtu ananihitaji basi tuwasiliane nipo sina shaka."
Madai hayo yamekuja baada ya serikali ya Marekani kutangaza kitita cha dola $10 million kwa mtu atakaye toa habari zitakazo fanya kukamatwa kwa Mohammad Saeed ambaye Marekani inasema alihusika katika milipuko ya ugaidi ya mwaka 2008 na kuu watu 166.

Rais wa Malawi alazwa hospitali.


Blantyre, Malawi - 05/04/2012. Rais wa Malawi amelazwa hopsitali baada ya kukutwa na matatizo ya ugonjwa wa moyo.
Rais Bingu wa Mutarika 78 alianguka wakati akiwa katika shughuli zake za kiserikali.
Kwa mujibu wa habari kutoka ofodi ya rais zimasema " kumekuwa na mshituko mkubwa kwani nchini nzima kutokana na tukio hilo."
Malawi ni nchi ambayo imekumbwa na misukosuko ya kiuchumi kwa muda sasa na hasa pale mauaji ya watu 19 yalipo tokea mwaka 2011 na kusababisha nchi za Ulaya Magharibi kulaani kitendo hicho  na nyingine kupunguza misaada kwa kudai serikali ya Malawi ifanye mabadiriko haraka  iwezekanavyo.




No comments: