Monday, April 2, 2012

Senegal yapata rais wa nne tangu kupata uhuru.

Miaka 30 yatimia tangu vita vya Falkland.

London, Uingereza - 02/04/2012. Miaka 30 imefikia leo tangu Uingereza kuvamia visiwa vya Falklands, ilikuling'o jeshi la Argentina lililo chukua kisiwa hicho.
Katika kuadhimisha kumbukumbu hiyo, waziri mkuu wa Uingereza David Cameron alisema "leo ni siku ya kuwakumbuka wale wote waliopoteza maisha katika vita hivyo, na Uingereza itaendelea kuwalinda Wanafalkland hadi hapo watakapo amua wao wenyewe.
Naye rais wa Argentina Christina Fernandez alisema "kitendo cha Uingereza kuendelea kukishikilia kisiwa hicho ni kinyume cha sheria na lazima wakiachie kisiwa hicho ni cha Argentina."
Mvutano wa Argentina na Uingereza zimekuwa zikivutana nani anamiliki kisiwa hicha kwa muda sasa jambo ambalo halijapatiwa jibu.


Chama cha Aung San Kyi chashinda viti vya bunge. 


Myanmar. Naypyitaw - 02/04/2012. Chama cha mwana harakati wa mapinduzi ya kisiasa nchini Myanmar kimetapa ushindi mkubwa katika uchaguzi uliyo fanyika hivi karibuni.
Chama cha Aung San Kyi NLD-National League for Democrcy kilipata viti 44 katika uchaguzi huo.
Aung San Kyi alisema " huu ni mwanzo wa mageuzi nchini mwetu, vita bado vinaendelea ili kuleta haki na usawa, na tunamatumaini ya kuwa ushindi huu utaliwezesha bunge kufanya kazi kwa manufaa ya wananchi."
Katika harakati za uchaguzi huo serikali ya Mynmar imedai ya kuwa uchaguzi ulikuwa wa haki na wasimamizi wa kimataifa waliruhusiwa kuangalia uchaguzi huo unakwenda kihalari.


Senegal yapata rais wa nne tangu kupata uhuru.


Dakar, Senegal - 02/04/2012. Wananch wa Senegal wameoata rais mpya, ambaye amepishwa wiki moja baada ya matikeo ya uchaguzi kutolewa.
Macky Sall 50, aliapishwa kuwa rais wa Senegal baada ya kumshinda aliyekuwa rais wa nchi hiyo Abdullaye Wade katika uchaguzi uliofanyika mara ya pili baada ya uchaguzi wa kwanza kutotoa mshindi.
Macky Sall alishinda uchaguzi huo kwa kupata kura asilimia 66% na Wade alipata asilimia 34%.


Serikali ya Syria yakubaliana na Koffi Annan.


Damascus. Syria - 02/04/2012. Serikali ya Syria imekubaliana na mpango wa amani uliopendekezwa na mwakilishi wa umoja wa mataifa Koffi Annan.
Rais wa Bashar al Assad, amekubaliana ya kuwa tarehe 10/April itakuwa siku ya kuanza mpango mzima wa kusimika muhimiri  amani uliyo pendekezwa.
Koffi Annan ambaye ni msimamizi wa kuleta amani nchini Syria alisema " lazima kamati ya ulinzi ya umoja wa Matifa ifikirie mpango wa kuandaa wajumbe ambao watakuwa na majukumu ya kusimamia na kuangalia hali ya usalama.
Mpango huo ambao  wa 10/April unatarajiwa kutoa ruhusa kuwepo kwa amani na jeshi la Syria litaanza kutoka katika miji ambayo ipo chini ya jeshi hili.

No comments: