Monday, April 16, 2012

Tanzania moja ya nchi itakayo simamishiwa misaada na Kanada

Mshitakiwa wa mauaji ya kustisha nchini Norway afikishwa mahakamani.

Oslo, Norway - 16/04/2012. Mtuhumiwa  aliye husika katika mauaji ya kutisha ya kihistoria nchini Norway amefikishwa mahakamani kujibu mashitaka yanayo mkabili.
Anders Behring Breivk 33 alifikishwa mahakamani ili kujibu mashitaka ya mauaji ya watu 77 aliyo yafanya mwaka 2011 Julai.
Akijibu baada ya kusomewa mashitaka yake Anders Breivk alisema " natambua kitendo nilicho fanya, lakini sioni kama ni kosa, kwaini nilikuwa najitete kwa kujilinda na kitendo cha Waislaam kuivamia Ulaya, na si itambui mahakama hii kwani mmepata maagizo kutoka kwa serikali ambayo ina unga mkono mchanganyiko wa watu kutoka sehemu tofauti na dini zao."
Hata hivyo Wanorway walio wengi wanahisi yakuwa Anders Breivk atatumia mahakama hiyo ili kukuza  itikadi za watu wa lengo wa kulia wanao pinga wageni na Waislamu na hasa kupitia majarida 1,500 ambayo yalichapishwa kwenye mitandao kabla ajafanya mashambulizi hayo.
Kwa mujibu wa wansheria wa Norway wanadai yakuwa Anders Behring Breivk ikiwa atakutwa na hatia huenda akahukumiwa kwenda jela miaka 21 ambayo huenda ikaongezwa na akakaa jela maisha.


Tanzania moja ya nchi itakayo simamishiwa misaada na Kanada.


Dar - es- Salaam, Tanzania - 16/04/2012. Tanzania itakuwa moja ya nchi ambazo zitakumbwa na hatua ya serikali Kanada kuamua kusimamisha kutoa misaada kwa kipindi cha miaka mitatu.
Serikali ya Kanada imeamua kusimamisha utoaji wa misaada hiyo ya kifedha yenye thamani ya dola million 400 za Kimarekani kupitia mpango unaojulikana CIDA - Canadian International Development Agency
Habari kutoka serikali ya Kanada zinasema "nchi zote  ambazo zina husika katika mradi huo zitafahimishwa kuhusu uamuzi huo siku chache kuanzia sasa."
Nchia  nyingine ambazo zitaathirika na kusimamishwa kwa kutolewa misaada hiyo ni Afghanistan, Bolivia, Mozambique na Pakistan.


Boko Haram kutishia kuangusha serikali ya Goodluck Jonathan.


Lagos, Nigeria - 16/04/2012. Kundi linalo pingana na serikali ya Nigeria na lenye itikadi kali ya kidini nchini Nigeria limetishia kuiangusha serikali ya nchi hiyo.
Mmoja wa viongozi kundi hilo Boko Haram alisema katika video ilyopatika " tutaiangusha serikali ya Goodluck Jonathan katika kipindi cha miezi mitatu."
Tishio hilo limekuja baada ya serikali ya Nigeria kupata msukumo kutoka serikali ya Marekani ili kupambana na makundi ambayo yanaleta mvurugo wa amani nchi Nigeria.


Benki ya dunia yapata rais mpya.


Johannesburgh, Afrika ya Kusini - 16/04/2012.  Matumaini ya nchi za Afrika kupata rais wa benki hya dunia ya mefutwa,baada ya Dr Jim Yong Kim kuchaguliwa kuwa rais wa benki hiyo.
Dr Jim Yong Kim, raia wa Marekani mwenye asili ya kutoka  Korea, alichaguliwa na kuwaacha wapinzani wake walio kuwa wakigombea kiti hicho kwa udadisi mkubwa.
Bara la Afrika lili kuwa limempendekeza Bi Ngozi Okonjo Iweala ambaye ni waziri wa Afya wa Nigeria kugombea kiti hicho, lakini hakufanikiwa kutoka na upinzani ulikuwepo katika kinyanganyiro hicho cha kugombea kazi ya juu ya kimataifa katika kusimamia mswala ya fedha.
Kabla  ya matokeo hayo, Bi Okonjo Iweala alisema " uchaguzi wa urais wa benki ya dunia haukufanyika kimsingi."
Uongozi katika benki ya dunia umekuwa ukielezewa ya kuwa unaupendeleo wa aina fulani kwa uongozi huo huwa unapelekwa kwa nchi zilizoendelea, jambo ambalo linatoa mthiani kwa bara la Afrika na uongozi wake.

Umoja wa Mataifa walaani kitendo cha Korea ya Kaskazini kukiuka sheria za kimataifa.


Washington, Marekani - 16/04/2012. Kamati ya usalama ya umoja wa Mataifa imelaani kitendo cha Korea ya Kaskazini kurusha roketi kinyume cha sheria.
Laana hiyo kutoka katika kamati ya usalama ya umoja wa Matifa, imekuja baada mtambo wa kisayansi wa Korea ya Kaskazani kuharibika baada ya kurushwa hivi karibuni.
Kamati hiyo ya usalama ya umoja wa Mataifa ilisisitiza pia vikwazo lazima viwekwe kwa viongozi na makampuni yaliyopo Korea ya Kaskazini,ili kuifanya serikali ya Korea ya Kaskazini kubadili msimamo wake wa kinyuklia.
Mvutano wa kinyuklia kati ya  nchi za Magharibi na hasa Marekani kwa kudai yakuwa Korea ya Kaskazini ilikuwa na mpango wa kurusha roketi ili baadaye wajaribu bomu la nyuklia.

No comments: