Tuesday, April 24, 2012

Mahakama ya kutetea haki za binadamu kuichunguza Mali.

Waumini wa dini ya Kiislaamu hawapatiwi haki zao vyema barani Ulaya. 


London, Uingereza - 24/04/2012. Shirikisho la kimataifa la  kutetea haki za binadamu Amnesty International limedai ya kuwa waumini wa dini ya Kiislaam wanabaguliwa katika baadhi ya nchi za ulaya.
Katika repoti yake Amnesty International ilisema " Watu wenye imani na dini ya Kiislaam wamekuwa na wakati mgumu katika nyanja za elimu, zakikazi na hata kuwa vigumu kupata maeneo ya kusalia.
"Ubaguzi huu ambao ni wakunuiwa juu wa Waislaam hupo hasa katika nchi za Switzerland,Ufaransa, Spain,,Beligium na Uhollanzi.
Marco Perolini mtaalamu wa mambo ya jamii na ubaguzi katika shirikisho hilo aliongeza kwa kusema "Ubaguzi huu umekuzwa na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa katika kila kampeni za uchaguzi ili kupata kura na inajulikana ya kuwa sheria ilisha pitishwa na muungano wa nchi wanachama wa jumiya ya Ulaya  ya kuwa ni mafuku kumbagua mtu kwa kupitia dini, rangi na imani lakini sheria hiyo imekuwa haina nguvu katika nchi wanachama."
Mvutano wa dini, wageni na imani zao katika nchi za Ulaya umekuwa ukitumiwa na wanasiasa wengi hasa katika kampeni za kutaka kura katika kipindi cha miaka ya karibuni, jambo ambalo limekuwa linaleta hali ya wasiwasi kwa baadai ya wageni waamiaji na wenyeji.

Serikali ya Izreal kuendelea na ujenzi wa makazi.


Jerusalemu, Izrael - 24/04/2012. Serikali ya Izrael imepitisha muswada wa kuruhusu ujenzi wa makazi katika maeneo ambayo Palestina inadai ni ya Wapalestina.
Waziri Mkuu wa Izrael Benjamin Netanyahu alisema " uamuzi wa kujenga makazi katika maeneo ya Sansana, Rechelim na Bruchin yalipitishwa na serikali iliyo pita."
Hata hivyo Benjamini Netanyahu hakueleza kwa kirefu kuhusu uamuzi huo wa kuruhusu ujenzi wa makazi.
Saeb Erekat mwakilishi katika majadiliano ya kuleta amani kati ya Wapalestina na Waizrael alisema " serikali ya Izrael inabidi ichague amani au kuendelea na ujenzi wa makazi katika maeneo ya Wapalestina.
"Swali ni kwamba ikiwa kuna watu wanasema kuwe na mataifa mawili  majirani ya Wapalestina na Waizrael mbona ujenzi wa makazi bado unaendelezwa?
Nafikiri uamuzi wa kuendelea kujenga maeneo hayo kuna vuga mpango mzima wa kuleta amani."
Mazungumzo kati ya Wapalestina na Waizrael yamesimama baada ya viongozi wa Palestina kukataa kuendelea na mazungumzo kwa madai ya kuwa serikali ya Izrael isimamishe ujenzi wa makazi katika maeneo inayo yashikilia.

Mahakama ya kutetea haki za binadamu kuichunguza Mali.


Hague, Uhollanzi - 24/04/2012. Mahakama ya kimataifa inayo shughulikia kezi za ukiukwaji wa haki za binadamu na mauaji ya raia inaaangalia na kufuatiilia kiundani kama makoso ya ukiukwaji wa haki za binadamu yalifanyika nchini Mali wakati wa mapinduzi ya kuing'oa serikali ya nchi hiyo.
Habari zilizo patikana kutoka ofisi ya mwanasheria mkuu wa mahakama hiyo zinasema " kunauwezekano mkubwa makosa ya ukiukwaji wa haki za binadamu yalifanyika, na ndo maaana inabidi uchunguzi ufanyike ili kujua ukweli."
Mali imekuwa na mvurugiko wa amani mara baada ya jeshi kuipindua serikali ya rais Amadou Toumani Toure na wakati huo huo  watu wa kabila la Taureg  wengi wao waliopo kaskazini mwa Mali wanataka nchi  igawanyike na wawe huru kutoka  serikali kuu ya Bamako.

Iran yazidi kujijenga kisiraha na nguvu za kijeshi.


Tehran, Iran - 24/04/2012. Jeshi la serikali ya Iran limedai yakuwa linauwezo wa kijeshi wa kulinda nchi ya Iran kwa kila namana na pia kuongezea ya kuwa siku si nyingi watazindua siraha ya kijeshi yanye uwezo wa kwenda mwendo wa kasi wa mita 100 kwa sekunde.
Kamanda wa jeshi hili  Rear Admiral  Ali Fadavi alisema " Iran itakuwa nchi ya pili kwa kuwa na uwezo huo wa kuwa na siraha ya kivita yenye uwezo wa kusari ndani ya maji kwa kasi ya mita 100 kwa sekunde.
Iran haita tikiswa na maadui zake kwani mafanikiyo yote ya kujilinda ni juhudi za wanasayansi wazalendo."
Mkuu huyo wa jeshi aliyasema hayo wakati wa uzinduzi wa mizinga aina ya IRGC uliyo fanyika hivi karibuni.
Serikali ya Iran imekuwa ikishutumiwa na nchi za Ulaya Magharibi na Marekani kwa kuwa na nia ya kutengeneza siraha za kinyuklia, jambo ambalo Iran imekuwa inakanusha kwa madai yakuwa mradi wa kinyuklia ni kwa ajili ya maendeleo ya kisanyansi.

No comments: