Sunday, April 29, 2012

Bomu lalipuka kanisani jijini Nairobi.

Uingereza kuimarisha ulinzi kabla ya michezo ya Olyimpiki jijini London.


London, Uingereza - 29/04/2012. Serikali ya Uingereza imetangaza ya kuwa itaweka mizinga ya kurushwa hewani na majini ikiwa katika harakagti za kuimarisha usalama kabla ya kuanza kwa mashindano ya Olimpiki hivi karibuni.
Mmoja wa mkazi wa jiji la London Brian Whelan alisema " nimeshtuka saana baada ya kujua karibu na maeneo tunayoishi yatafungwa mkitambo hiyo ya kijeshi, kwani eneo hili liona majengo mengi saana nasijui itakuwaje?
"Na ni kweli kuna swala la usalama jambo ambalo linabidi litizamwe kwa makini na linaleta mshawasha."
  Wizara ya ulinzi ya Uingereza imeamua kuweka mitambo hiyo ili m,kuweza kuimarisha usalama wa jiji la London ikiwa kutatokea majaribio ya mashambulizi ya ya kigaidi ya anga au majini.

Bomu lalipuka kanisani jijini Nairobi.


Nairobi, Kenya - 29/04/2012. Bomu limelipuka ndani ya kanisa wakati misa inaendelea jijini Nairobi na kusababisha kifo cha mtu mmoja na wengine kumia kijeruhiwa vibaya.
Mashambulizi hayo ambayo yalitokea katika kanisa lijulikanalo kama Nyumba ya Maajabu ya  Mungu katika kitongoji kijulikanalo kama Ngara.
Mmsemaji wa polisi Eric Kiraithe alisema "polisi wana habari ya kuwa mashambulizi hayo yametokea  na  bado wanaendelea na uchunguzi."
Jiji  la Nairobi limekuwa linakumbwa na mashambulizi ya mabomu, tangu kundi la Al Shabab la Somalia kutangaza ya kuwa wataishambulia Kenya kwa hali na mali, kutokana na kitendo cha jeshi la Kenya kuingilia kati mambo ya ndani ya Somalia na kuanzisha mashambulizi nchini Somalia.


Meli yakamatwa na siraha za wapinzani wa Syria.


Beiruti, Lebanoni - 29/04/2012. Serikali ya Lebanoni imekamata meli iliyo kuwa na na siraha ambazo zinasadikiwa zilikuwa zinaelekea kwenye kambi ya wapinzani wa serikali ya Syria.
Milos Strugar ambaye ni msemaji wa (UNIFIL) United Interim Force in Lebanon alisema " tumeweza kuizua meli hiyo ikiwa ni moja ya kazi zetu kuzuia uingizaji wa siraha kinyume cha sheria."
Meli ili ambayo imezuiliwa na mabaharia wake  11 imesemekana na ya kuwa meli hiyo imetokea nchini Libya ambapo kuna maghala ya siraha ambazo zilikuwa zimetumika katika kuuong'oa utawala wa Muammar Gaddafi.
Ofisi ya  mmiliki wa meli hiyo alisisitiza ya kuwa waliambiwa ya ,kuwa meli hiyo ilikuwa imeba mashine za mafuta na kwa mujibu wa sheria hawana ruhusa kufungua makontena hayo kuangalia ndani ,kuna nini.

No comments: