Friday, April 13, 2012

Mtambo wa Korea ya Kaskazini washindwa kufika mwezini.

Serikali ya Baraka Obama kuimarisha vitega uchumi barani Afrika.

Washington, Marekani - 13/04/2012. Wachumi,wafanyabiashara na wanasiasa wa Marekani wameitaka serikali izidishe kuwekeza vitega uchumi katika bara la Afrika.
Maagizo hayo yamekuja baada ya muswada kupitishwa ili kuimarisha na kuzidisha vitega uchumi katika bara la Afrika na kusema  "kwani kwa kufanya hivyo kutaimarisha uhusiano kati ya Waafrika na Wamarekani."
Uamuzi huo wa kupitishwa muswada huo wa kuwekeza vitega uchumi barani  Afrika umekuja ili kuweza kuikabili China ambayo imeisha jiweza na kuimarika katika bara la Afrika kwa muda sasa.
Muswada huo ambao umepitishwa katika serikali ya Baraka Obama utafatilia miswada mingine iliyopitishwa wakati wa utawala wa George Bush na Billy Clinton ambapo serikali hizo zilipitisha miswaada ya kiuchumi na kiutu ili kuimarisha maisha ya watu wa Afrika na kuinua uchumi kwa jumla.

Hali shwari nchini Syria na UN kupeleka wawakilishi wake.

Damascus, Syria - 13/04/2012. Umoja wa Mataifa umechagua watu 30 ambao watakwenda nchini Syria, ili kusimamia hali ya amani nchini humo.
Wawakilishi hao  ambayo bado kutajwa, watakuwa nchini Syria ili kuhakikisha amani inakuwepo na kusimamia mpango mzima wa majadiliano ya kisiasa " alisema Kofi Annan ambeye ni mwakilishi mkuu wa umoja wa Mataifa katika kusuruhisha ugomvi kati ya serikali ya Bashar al Assad na wapinzani ambao wanasaidiwa na nchi marafiki wanao pinga serikali ya Assad.
Leo ni siku ya pili tangu mswada wa kusimamisha mapigano kati ya majeshi ya serikali na ya upinzani  kutimizwa, baada ya Kofi Annan mwakilishi wa umoja wa Matifa kuzitaka pande zote mbili kuachana na mapambano ya kivita na kukaa chini kujadiliana kuhusu hali haya kisiasa na demokrasia ambayo itawanufaisha wa Syria wote.

Rais Robert Mugabe hana matatizo ya kiafya. 


Harare, Zimbabwe - 13/04/2012. Rais wa Zimbabwe amerudi Zimbabwe baada ya  ziara isiyo ya kiserikali nchini Singapore.
Kurudi huko kwa rais Robert Mugabe, kumetuliza habari zilizo kuwa zimeenea kuhusu hali yake ya kiafya, ambapo ili semekena ya kuwa " alikuwa anaumwa sana na yupo huko kwa matibabu."
Waziri wa habari Webster Shamu alisema " nafikiri mumemwona rais yupo imara kama chuma cha pua, nafikiri kutangaz habari za uongo siyo vizuri na tunajua hizi ni mbinu za mabepari."
Rais Robert Mugabe aliambatana na mkewe Grace huku Singapore ambapo habari kutoka serikalini zilisema " rais yupo huku kwaajili ya kuashughulikia maswala ya shule ya mtoto wake Bona."
Mugabe alionenekana akicheka na kufurahi na viongozi waliokuja kumpokea wakatia alipo wasili nchini Zimbabwe jana.


Mtambo wa Korea ya Kaskazini washindwa kufika mwezini.


Pyong Yang, Korea ya Kaskazini - 13/04/2012. Serikali ya Korea ya Kaskazini imekili ya kuwa mtambo a kisanyansi ambao waliurusha angani kwenda mwezini umeharibika kabla ya kufika huko.
KCNA-Shirika la habari za Korea ya Kaskazini liripoti "mtambo ambao ulirushwa angani umeshindwa kufika  baada ya kutokea matatizo ambayo hayajajulikana na kuanguaka baharini.
Wataalamu wameanza uchunguzi wa chanzo cha kuanguka kwa mtambo huo."
Mtambo huo ulikuwa umerushwa ili kumbatana na miaka 100 ya shereha ya kuzaliwa kiongozi mwasisi wa Korea ya Kaskazini Kim Ill Sung na kumkumbuka kiongozi mwingine Kim Ill Jung ambaye alifariki mwezi  Desemba 2011.



No comments: