Friday, April 6, 2012

Jeshi la China latakiwa kupuuzia uvumi wa kisiasa.

Rais wa Malawi Bingu wa Mutharika afariki dunia.


Blantyre, Malawi - 06/04/2012. Rais wa Malawi amefariki dunia baada ya kuupata matatizo ya moyo siku ya Alhamisi 05 April wakati akiwa katika shughuri zake za kiofisi.
Bungu wa Mutharika 78 ambaye alichaguliwa kuiongoza Malawi mwaka 2004 na kuchaguliwa tena kwa mara ya pili mwaka 2009 kuwa rais wa  Malawi na mwaka 2011 kukumbwa na mvutano wa kisiasa na Uingereza hivi karibuni jambo ambalo lilisababisha uhusiano kati ya Malawi na Uingereza kudorola.

Watuareg wajitangazia uhuru ndani ya Mali.

Timbuktu, Mali - 06/04/2012. Kikundi la upinzani lililopo nchini Mali la Tuareg limetangaza kujitawala badaa ya kuchua eneo kubwa nchini Mali.
Kundi hili linalo julikana kama (MNLA)-The National Movement for the Liberation of Azawad ambalo lilifanikiwa kuchukua eneo kubwa nchini Mali, lili tangaza ya kuwa linataka lijulikane kama "Azawad."
Hata hivyo Umoja wa Afrika umepinga swala hilo na kuagiza kuwa jumjuiya ya kimataifa kutokubaliana na kundi hilo.
Nayo serikali ya Ufaransa imeunga mkono ombi la Umoja wa Afrika na kusema "Ufaransa haitaitambua ombi hilo la MNLA na Mali ni nchi moja na tunataka Mali kuwa nchi moja.

Mahakama ya Hague ya Uhollanzi yamtaka Saif al-Islaama Gaddafi. 

Hague, Uhollanzi - 06/04/2012.  Mahakama inayo shughulikia makosa ya jinai na kutetea haki za binadamu iliyopo Uhollanzi imetaia serikali ya Libya kumpeleka mtoto wa Muammar Gaddafi nchini Hollanzi.
Mahakama hiyo ya Hague ambayo ilitoa hati ya kukamatwa Saif al-Islaam Gaddafi ambaye yupo chini ya mikono ya serikali ya mpito ya Libya tangu alipo kamatwa  mwaka 2011 Novemba wakati akiwa katika harakati za kutoroka.
Naye mwanasheria anaye mtetea Saif al-Islaam Gaddafi alisema " tangu Saif kakamatwa amekuwa ananyanyaswa, kunyimwa haki zake na kufungiwa kwenye vyumba vya giza."
Serikali  ya Libya imekuwa ikivutana na mahakama ya Hague, kwa madai wanataka kesi dizi ya Saif al-Islaam Gaddafi  ifanyike nchi Libya.

Wakuba washerekea kwa mara ya kwanza sikukuu ya Ijumaa Kuu tangu mwaka 1959.

Havana, Kuba - 06/04/2012. Wanchi wa Kuba wamesherekea kwa mara ya kwanza siku ya kumbukumbu ya kuteswa kwa Yesu Kristu msalabani.
Siku ya Ijumaa Kuu siku ambayo haikuwa katika sikukuku za serikali ya Kuba kwa muda wa miaka mingi, ilisherekewa na waumini wa dini ya Kikristu wa Kuba, baada ya Papa Benedikt XVI kuiomba serikali ya kuitambua rasmi siku hiyo.
Ombi hilo la Papa limefuatia ombi la kwanza lililo fanywa na marehemu Papa John Paul II aliye iomba serikali ya Kuba kufanya siku ya kuzaliwa kwa Yesu Kristu - Krismas kuwa siku ya mapumziko na kusherehekewa kitaifa.
Serikali ya Kuba ilipiga marufuku sikukuu za kidini mwaka 1959 baada ya kufanyika mapinduzi.


Jeshi la China latakiwa kupuuzia uvumi wa kisiasa.


Pyong Yang - China - 06/04/2012. Jeshi la China limewataka wanajeshi nchini humu kutilia maanani swala la ulinzi wa nchi na kuachana na uvumi ya kuwa kulikuwa kuna mpango wa kufanywa mapinduzi.
Habari hizi zimetolewa na gazeti la jeshi la China, kwa kuripoti " wanajeshi wa China wanatakiwa kuzuia na kulinda propaganda za aina yoyote, kwani zinaleta kelele zisizo na maana na hazitasaidia lolote kwa ni uvumi wa kisiasa."
Wanchi wa China wana tarajia kuona mabadiliko ya uongozi wa kisasa kabla ya mwisho wa mwaka huu.

No comments: