Tuesday, August 4, 2009

Nashukuru kuondoka kwa Eto'o,alikuwa ananipa ndoto zisizo za kawaida.

Nashukuru kuondoka kwa Eto'o, alikuwa ananipa ndoto zisozo za kawaida.

Madrid, Uispania - 04/08/09. Golikipa au mlinzi namba moja wa timu ya taifa ya Uispania Iker Casillas, amesema amefurahi kuondoka kwa mshambuliaji hatari wa timu ya FC Barcelona na timu ya taifa ya Kameroon, Samwel Eto'o.
Akiongea leo hii, Casillas, alisema ya kuwa Eto'o, alikuwa akimfanya aote ndoto zisizo eleweka kila anapo fikilia mechi na timu ya Barcelona.
Akiulizwa na waandishi wa habari, Iker Casillas, kuhusu mshabuliaji ,Zlatan Ibrahimovic, mlinda mlango huyo, alisema Ibrahimovic ni mchezaji mzuri, lakini Eto'o ni hana mfano.
Hapo juu, ni picha tofauti, zinaonyesha ni kwa kiasi gani,mlinzi wa timu ya Madrid, Iker Casillas, alivyokuwa akiteswa na kuteseka kila anapo kutana na mshambualiji wa Barcelona, Samwel Eto'o.
Kwani, Eto'o amekuwa akimpa wakati mgunga mlizi huyo, Iker Casillas na kuona nyavu zilizo chini ya ulinzi wa kipa huyo.

No comments: