Wednesday, August 19, 2009

Mmea wa bangi majaribioni kutibu kansa.

Rais wa za zamani wa Zambia, ashukuru Mungu, "Kesi imefutwa" Lusaka, Zambia - 19/08/09. Rais wa zamani wa Zambia, Frederick Chiluba, ameachiwa huru, baada ya kukutwa hana hatia ya kula rushwa wakati wa uongozi wake akiwa rais wa Zambia. Kesi hiyo, ambayo aliyo kuwa inamkabiri rais huyo wa zamani wa Zambia, Fredrick Chiluba ni kuhusika na upotevu wa $500,000 za Amerika Kwa mujibu wa mahakama, wanasheria wa serikali walio fungua kesi hiyo walikosa ushahidi kamili. Rais huyo wa zamani wa Zambia, Fredrick Chiluba, amekuwa akikabiliwa na kesi iliyo chukuwa miaka minane tangu ashitakiwe. Mungu ni mkubwa, ameonyesha ukweli upo wapi na alisikika akisema hayo rais huyo wa zamani wa Zambia. Picha hapo juu, anaonkekana, rais wa zamani wa Zambia, Fredrick Chiluba, akinyanyua mikono juu kumshukuru Mungu, mara ya kusikia kesi iliyo kuwa ikimkabili imetupiliwa mbali na mahakama. Wanaume wabakwa kwa wingi nchini DRC. Goma, DRC - 19/08/09. Hali imezidi kuwa mbaya katika eneo la Goma, baada ya wanaume kuanza kubakwa. Kwa mujibu wa mmoja ya watu waliokumbwa na mkasa huo,Kazungu Ziwa,alisema alivamiwa na kukamatwa na watu wenye mapanga na virungu. Baada ya kuvamiwa alijaribu kupigana nao, lakini alishindwa , na matokeo ya ke wakamtawiti kwa nguvu, na baadaye walimwacha akiwa taabaani. Kwa mujibu wa bwana Ziwa, alisema ya kuwa watu hao, walikuwa ni moja ya makundi wanaopigana katika maeneo hayo. Picha hapo juu, ni moja ya picha za watu ambao walikumbwa na mikasa ya kulawitiwa.

Mmea wa bangi majaribioni kutibu kansa.
London,Uingereza -19/08/09.Mmoja wa wataalamu wanaofatilia tiba ya kansa,Ine Diaz-Laviada, amesema ya kuwa mmea wa bangi unaweza kusaidia kuponyasha ugonjwa wa kansa.
Ine Diaz Laviada, alisisitiza ya kuwa chunguzi wa muda mrefu umeonyesha mmea huu unaweza kutumika kama dawa ya kusaidia kutibu kansa.
Hata hivyo bado uchunguzi unaendelea zaidi.
Picha hapo juu, ni ya mmea wa bangi, mmea ambao huenda hapo baadaye ukasaidia kutibu kansa.
Mwanafunzi mzee kuliko wote, afariki dunia.
Nairobi, Kenya - 19/08/09. Raia wa Kenya, Mzee, Kimani Nganga Maruge aliyekuwa na miaka 90, amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu ugonjwa wa kansa ya tumbo.
Mzee Kimani Nganga Muruge, ambaye aliweka historia,na kuandikwa katika kitabu cha historia, kwa kujiandikisha shule ya msingi huku akiwa na miaka 84,na mzee wa kwanza kuanza shure akiwa na umri mkubwa.
Mzee, Kimani Nganga Magure, aliamua kujiandikisha shule,baada ya kuhisi ya kuwa muhubiri alikuwa anatafsili vibaya na kupoteza maana ya ujumbe kamili.
Mzee, Kimani Nganga Maruge, alikuwa mmoja ya wapigania uhuru wa Kenya miaka ya 1950, chini ya Uongozi wa Mau Mau.
Picha hapo juu, anaonekana katikati mzee Kimani Nganga Maruge,akiwa darasani na yupo tayari kuuliza swali.Mungu ailaza mahari pema peponi roho yake mzee Kimani Nganga Maruge.
Wajenzi wa viwanja kupata tiketi za bure, " Mchezo wa soka Afrika ya Kusini.
Johannesburg, Afrika ya Kusini -19/08/09. Chama cha mpira nchini Afrika ya Kusini, kwa kushirikiana na shirikisho la kandana ulimwenguni FIFA, zimepanga kutoa tiketi zaidi ya 120,000 za bure, ili waler wapenzi wa sika nchini humo, wasio na uwezo wa kulipa waweze kuhudhulia mashindano hayo ya soka yatakayo fanyika nchini humo - ( Afrika ya Kusini).
KWa mujibu wa FIFA, tiketi hizo za bure, zitadhaminiwa na mashirika na makampuni ya Adidas,Coca Cola, kampuni ya Magari ya KIA, Emarates, Hyundai, Sony na Visa.
Kufuatia kutolewa kwa tiketi hizo, wajenzi wote waliohusika katika kujenga viwanja hivyo, watakuwa wa kwanza kupata tiketi hizo.
Picha hapo juu ni ya mmoja ya washibiki wa soka nchini Afrika ya Kusini, ambaye huenda akabahatika kupata tiketi ya bure kuona mpambano wa soka wa kunyanyia kombe la Dunia.

No comments: