Monday, August 3, 2009

Katibu mkuu wa NATO aanza kazi rasmi.

Mfereji wa Suezi wa kumbwa na upepo wa kiuchumi. Suez Kanal, Misri - 03/08/09. Serikali ya Misri imesema ya kuwa kutokana na hali ya uchumi kuyumba na vitendo vya ugaidi kuzidi katika bahari za Hindi ,kumefanya mapato ya kodi kushuka kwa kiasi kikubwa na kufikia asilimia 7.2 (7.2%). Mfereji wa Suez, unatumika kwa kupitishia meli zote, zinazo ingia na kutoka bara la Ulaya na Amerika kuelekea bara la Asia, Afrika na nchi za Mashariki ya kati. Akiongea haya, mkuu wa mfereji huo wa Suez, Ahmed Ali Fadel,alisema yakuwa matatizo ambayo yanaikumba dunia kiuchumi yanachangia kwa kiasi kikibwa, anaamini hali ya mapato ya kodi yataanza kupanda hapo hali ya uchumi itakapo kuwa nzuri. Picha hapo juu, nimoja ya boti ya polisi, ikiwa katika ulinzi wa mfereji wa Suez, ambapo kwa kipindi hiki, meli zimekuwa hazipiti kwa wingi kwa sababu tofauti, moja wapo swala la usalama katika pwani karibu na Somalia.

Katibu mkuu mpya wa NATO, aanza kazi rasmi.
Brussel, Ubeligiji 03/08/09. Katibu mkuu mpya wa NATO, Fogh Rasmussen,ambaye pia alishawahi kuwa waziri mkuu wa Denmark,ameanza kazi rasmi leo.

Kabla ya kuanza rasmi kazi ya ukatibu mkuu wa NATO leo, amesema wakati wa uongozi wake , atahakikisha ya kuwa Afghanistan, wanakuwa na ulinzi wao wenyewe na kulinda usalama wa nchi yao, na hivyo kuzitaka nchi wanchama wa NATO, kushirikiana zaidi ili kufanikisha lengo hilo.

Aliongezea ya kuwa NATO, itazidisha ushirikiano na nchi wanachama wa jumuiya zanchi za Kiislaam.

Jumuiya hizo ni Mediteranian Dialogue (MD) na Istambul Co- operation Initiative (ISCI).

Fogh Rasmusessen, amechukua kazi iliyo achwa na katibu mkuu wa zamani wa NATO, Jaap de Hoop Sheffer.

Pichani hapo juu wanaonekana, Jaap Hoop Sheffer,ambaye anatoka madarakani kama katibu mkuu wa NATO na kulia ni katibu mkuu mpya wa NATO, Fogh Rasmussen,akiongea ni kwa jinsi gani wakati wa uongozi wake atakavyo fanya.

Picha ya pili, ni ya Katibu mkuu mpya wa NATO, Fogh Rasmussen, akiongea mbele ya wajumbe NATO.

No comments: