Thursday, May 3, 2012

Mtoto wa Muammar Gaddafi ataka Luis Moreno Ocampo kuchunguza kifo cha baba yake.

Urusi ya toa taadhari kwa ikiwa mitambo ya kijeshi itawekwa barani Ulaya na Marekani.


Moscow, Urusi - 03/05/2012. Serikali ya Urusi imesisitiza ya kuwa  inauwezo wakutumia nguvu zake za kijeshi na kushambulia mitambo ya kijeshi ya Marekani itakayo wekwa Ulaya.
Chief Generali Staff Nikolay Makarov alisema " ikiwa mitambo ya ABM ya Marekani itawekwa bila kufikia makubaliano na kusababisha hali ya usalama wa Urusi kuwa katika hali isiyo ridhisha, basi hakuna njia nyingine ni kuizuia kwa kutumia mbinu za kijeshi.
" Urusi haina mipango wa kuweka mitambo yake ya kivita nje ya nchi."
Mvutano kati ya Urusi na Marekani kuhusu kuwekwa kwa mitambo ya kijeshi ya Marekani barani Ulaya kwa madai yakuwa ni kwaajili ya kulinda usalama wa Marekani na washiriki wake zidi Iran, jambo ambalo Urusi inalitilia mashaka ya kuwa ni mmpango wa Marekani wa kutaka kukuza uwezo wa kijeshi barani Ulaya. 

Mtoto wa Muammar Gaddafi ataka Luis Moreno Ocampo kuchunguza kifo cha baba yake.

Algeirs, Algeria - 03/05/2012.  Mtoto wa kike  wa aliyekuwa rais wa Libya amemwandikia mwanasheria mkuu wa mahakama ya kimataifa kwa kutaka kesi ya ukiukwaji wa haki za binadamu ifunguliwe ili kuchunguza chanzo cha kifo cha baba yake mzazi.
Aisha Gaddafi ambaye yupo makimbiloni nchini Algeria alisema kupitia mwanasheria wake Nick Kaufman " ningependa kuchukua nafasi hii kuwakumbusha makubaliano ya Rome ambayo ndiyo msingi mkubwa wa Mahakama ya kiamtaifa inayaoshughulikia utetezi wa haki za binadamu  na naomba mwanasheria wa mahama hiyo  afanye uchunguzi wa kifo cha baba yangu Muammar Gaddafi na kufikisha swala hili kwa kamati ya usalama ya umoja wa mataifa."
Aisha Gaddafi ambaye pia ni mwanasheria amekuwa akisimamia swala la kutaka kufanyika uchunguzi wa kifo cha baba yake ambaye aliwawa baada baaada ya serikali yake kuangushwa na kundi la wapinzani kwa msaada wa NATO.

Serikali ya Marekani yatoa siri na mipango ya Osama bin Laden.

Washington, Marekani - 03/05/2012. Serikali ya Marekani imechapisha kwenye mitandao baadhi ya maelezo na mipango ambayo ilikuwa imeandaliwa na kiongozi wa kundi la Al Qaeda.
Maelezo hayo na mipango hiyo imechapishwa kwenye mtandao wa idara inayo simamia maswala kupigana na ugaidi Combating Terrorism Centre ikiwa ni moja ya  kurasa za maelezo 6,000 ambazo zilipatikana baada ya kumvamia kiongozi wa kundi hilo la Al Qaeda Osama bin Laden mwaka jana May 2011 nchi Pakistan na kumua.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema " maelezo yalipatikana kwenye faili za mitandao ya mtandao aliyokuwa akitumia Osama bin Laden."
Wakati huo huo baadhi ya wananchi wameendamani nchi Afghanistan katika kuadhimisha mwaka mmoja tangu kuuwawa kwa kiongozi wa kundi la Al Qaeda na jeshi la  Mareakani mwaka 2011 may.
Kutolewa kwa maelezo hayo kumekuja siku mbili baada ya  rais wa Marekani baraka Obama kumaliza kufanya ziara nchi Afghanistani na kusisitiza ya kuwa jeshi la Marekani litakabidhi maswala ya ulinzi wa Afghanistan kwa jeshi la nchi hiyo muda si mrefu.

No comments: