Sunday, January 2, 2011

Brazil wapata rais wa kwanza mwana mke.

Brazil wapata rais wa kwanza mwanamke. Brasilia, Brasil - 02/01/2011. Wananchi wa Brazil wameshuudia kuapishwa kwa rais mpya wa nchi yao, baada ya muda wa rais wa sasa Luiz Lula da Silva kumalizika. Dilma Rousseff aliapishwa mbele ya watu wapatao 70,000 wakiwemo wageni waalikwa kutoka nchi tofauti duniani. Rais Dilma aisema " nitajitahidi kulinda na kuendeleza yale yote ambayo rais Luiz Inacio Lula Da Silva aliyo fanya katika kuinua uchumi wa wanchi wa Brazil na kuinua kiwango cha kila mwanchi kiuchumi." Picha hapo juu anonekana rais wasasa wa Brazil Dilma Rousseff kushoto akiwa na rais aliye mwachia ofisi Luiz Inaci Lula da Silva kwa pamoja wakiwa wamenyanyua mikono mara baada ya kuapishwa kwa Dilma Rousseffe kuwa rais wa kwanza mwanamke. Urussi yaaanza kuiuzia China mafuta.

Moscow, Urussi - 02/1/2011. Serikali ya Urussi kupitia makampuni yake ya mafuta imeaaza kusafirisha mafuta nchini China.
Usafirishaji huo wa mafuta utapitia Mashariki ya Siberia ambapo mitambo ya kusafirishia mafuta imewekezwa na itakuwa na urefu km 50,000.
Igor Dyomin ambaye ni msemaji wa kampuni ya kusafirisha mafuta Transneft alisema mitambo hiyo itakuwa na uwezo wa kusafirisha tani zamafuta 43,000 kwa siku.
Urussi ni nchi ambayo ni moja ya nchi inayo uza zao la asili ya mafuta na gasi katika nchi mbalimbali za ulaya.
Picha hapo juu ni ya bomba la mafuta likielekea nchini China ambapo imeaanza kununua mafuta kutoka Urussi

No comments: