Saturday, January 15, 2011

Rais wa Tunisia akimbia nchi.

Rais wa Tunisia akimbia nchi.

Tuinis, Tunisia 14/01/2011. Rais wa Tunisia amekimbilia nchini za Uarabuni baada ya hali ya kisiasa kuwa katika hali mbaya kwa upande wa uongozi wake.
Zine El Abidine Ben Ali ambaye ametawala nchini Tunisia kwa zaidi ya miongo miwili na nusu alikimbia nchi huku hali ikiendelea kuwa mbaya kufuatia maandamano yalifanywa na wanchi wa Tunisia kupinga hali ya kiuchumi kuwa ngumu.
Kufuatia kuondoka nchi kwa rais huyo, spika wa bunge Fouad Mebezaa ameapishwa kuwa rais wa muda ili kuiongoza Tunisia mpaka hapo uchaguzi mpya utakapo fanyika.
Picha hapo juu anaonekana rais wa zamani wa Tunisia enzi zake wakati alipo kuwa akiwasalimia wananchi mara katika moja ya sheehe za kitaifa.

No comments: