Thursday, January 13, 2011

Wahaiti wakumbuka siku ya tetemeko la ardhi.

Wahaiti wakumbuka siku ya tetemeko la ardhi. Port au Prince, Haiti - 13/01/2011. Maelfu ya wananchi wa Haiti wamekutana katika jiji la Port au Price kukumbuka siku ambayo tetemeko la ardhi lilitkea na kupoteza maisha ya watu na kuleta maafa makumbwa kwa kila jamii kiuchumi na kiafya. Tetemeko hilo ambalo lilipoteza maisha ya watu wapatao 316,000 kupoteza maisha yao na wengine kujeruhiwa vibaya. Kwa mujibu wa mashirika tofauti yanayotoa misaada nchini Haiti yamesema " hadi kufikia sasa hali nchini humo bado siyo ya kulizisha na juhudu zinatakiwa kuongezeka ili kuijenga nchi hiyo na kuinua hali ya misha ya watu wake." Picha hapo juu ni misaraba ikiwa inawakilisha watu waliopoteza maisha wakati wa tetemeko la ardhi lililo tokea mapema mwaka 2010. Waamerika waombwa kuungana na kushirikiana. Tucson, Amerika - 13/01/2011. Rais wa Amerika amewataka Waamerika wote kuungana na kuishi kwa ushirikiano ijapokuwa kunatofauti za kisiasa. Rais, Baraka Obama aliyasemahayo wakati alipo udhulia siku maalumu ya kuwakumbuka watu walioshambuliwa kwa risasi na kupoteza maisha ya kwenye jimbo la Arizona. Baraka Obama alisema " mambo mabaya hutokea na nilazima tujitahidi kuwa wavumilivi hasa tukizingatia tumepoteza watu sita kutokana na ukatili uliofanyaka." Mtu anayehusika na mauaji hayo Jared Lougher 22 anashikiliwa kutokana na kufanya kitendo hicho cha kikatili. Picha hapo juu wanaonekana rais Baraka Obama akiwa na mke wake Micheel wakishika kwenye ndege kuelekea kuhudhulia siku maalumu ya kuwakumbuka watu waliopoteza maisha wakati wa mashambulizi ya kikatili.

1 comment:

Anonymous said...

Hellο, i think thаt i ѕаw you
viѕited my websitе thus i came to “return the fаѵor”.
I'm attempting to find things to enhance my site!I suppose its ok to use some of your ideas!!

Have a look at my site ... unlock iphone 3g