Wednesday, January 19, 2011

Ombi la kukamatwa kwa Tzipi Livni lakataliwa.

Odinga, Ouwattara na Gbagbo hakuna maelewano.

Abidjan, Ivory Coast-19/01/2011. Msuruhishi wa mgogoro wa kisiasa nchini Ivory Coast ambaye pia ni waziri mkuu wa Kenya ameondoka nchi humo bila kupata suruhisho la mgogoro huo.
Raila Odinga ambaye alipewa jukumu la kusuruhishwa mgogoro huo wa kisiasa aliwaambia waandishi wa habari ya kuwa imekuwa vigumu kufikia muaafaka kati ya pande zote mbili za kisiasa.
Akisisitiza Odinga alisema "muda wa mazungumzo ya hiyari unazidi kuwa finyu."
Hata hivyo msemaji wa serikali ya rais Laurent Gbagbo alisema "hatutakubali tena kuongea na Raila Odinga kwani anapendelea upande mmoja wa bwana Ouawattara na hatuko tayari kumpokea."
Picha hapo juu anaonekana Raila Odinga akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza mazungumzo na Laurent Gbagbo pichani kulia na Alassana Ouwattara pichani kushoto.
Amerika na China kushirikiana kwa karibu zaidi.
Washington, Amerika- 19.01/2011. Serikali ya Amerika na Uchina zimekubaliana kushirikiana katika usalama wa maswala ya kinyuklia na sekta za kibiashara. Kufuatia mikataba hiyo China itanunua ndege za aina ya boingi 200 na kuwekeza nchini Amerika vitega uchumi katika kilimo,mawasiliano. Wakiongea mbele ya waandishi wa habari marais hao walisema kukutana kwao kumeweka msingi mzuri ambao nchi zote mbili zitanufaika." Picha hapo juu wanaonekana rais wa Amerika Baraka Obama kushoto na rais wa China Hu Jintao wakiwasalimia wanchi waliokuja kuwalaki kabla ya kuanza mazungumzo rasmi kati yao jinsi ya kushirikiana kwa ukaribu zaidi. Watunisia watakiwa kuungana. Tunis, Tunisa- 19/01/2011. Rais wa kipindi cha mpito nchini Tunisia ametangaza yakuwa atahakikisha maswala yaliyo leta kutokuelewana na kunyanyasa wanachi hayatarudiwa tena na kutaka wanchi wa Tunisia kufungua ukurasa mpya. Fouad Mebazaa, akitangaza kupitia TV na vyombo vingine vya taifa na kimataifa alisema, sisi sote kwa pamoja tunaweza kuiongoza na kuijenga nchi yetu na hivyo tufungue ukurasa mpya ili kuijenga nchi yetu ambayo imeyumba kisiasa na kiuchumi." Hata hivyo bado kunahali ya mvutano wa kisiasa nchini Tunisia huku wanchi wakudai ya kuwa bado serikali hiyo inaviongozi waliokuwa wakati wa utawala wa rais Zine Ben Ali ambaye ameikimbia nchi baada ya wanachi kutaka atoke madarakani. Nayo serikali ya Swissi imezizuia mali zote za aliyekuwa rais wa Tunisia Zine Ben Ali. Picha hapo juu anaonekana rais wa mpito wa Tunisia Fouad Mebazaa akishuka kutoka kwenye gari, huku akiwa analindwa vikali na walinzi wake tayari kuelekea ofisini kuanza kazi rasmi ya kuongoza nchi. Ombi la kukamatwa kwa Tzipi Livni lakataliwa. Pretoria, Afrika ya Kusini- 19/01/2011. Serikali ya Afrika ya Kusini imekataa ombi la kutaka akamatwe aliyekuwa waziri wa mambo ya nchi za nje wa Izrael ambaye anatarajiwa kufanya ziara nchini humo. Ombi hilo lilitolewa na Shirika la Uhusiano la Wapalestina, kwa adai ya kuwa aliyekuwa waziri wa mamboya nje wa Izrael Tzipi Livni alihusika katika wakati jeshi la Izrael lilipo shambulia eneo la Gaza mwidho wa mwaka 2008 hadi mwanzoni mwa mwaka 2009. Mclntosh Polela ambaye ni msemaji wa ofisi ya usalama na makosa ya jinai alisema "tumepata ombi la kutaka kukamatwa kwa aliyekuwa waziri wa mambo ya njee wa Izrael na hatutachukua hatua hiyo na Tzipi Livni hatakamatwa kwani hakuna ushahidi wa kutosha zidi yake." Picha hapo juu ni ya Bi Tzipi Livni, ambaye alikuwa waziri wa mambo ya njee kati ya miaka ya 2009-9.
Mtoa siri za benki za Swisi ahukumiwa.
Zuriki, Uswisi - 19/01/2011. Mahakama jijini Zuriki imemkuta na makosa aliyekuwa mfanyakazi wa benki aliyehusika kutoa nyaraka za siri kwa Wikileaks ambazo zinaonyesha majina ya watu ambao wameweka pesa katika benki nchini humo.
Mshitakiwa huyo Rudolf Elmer alihukumiwa kwa kutozwa faini ya kiasi cha Swiss 7,200 ($7,505) na kuwa chini ya uangalizi kwa muda wa miaka miwili.
Akitoa hukumu hiyo hakimu alikataa ombi la mwasheria kwa upande wa mashitaka kwa kutaka adhabu ya kifungo itolewe kwa bwana Ridolf Elmer.
Rudolf Elmer alikubali makosa yake kabla ya hukumo hiyo kutolewa.
Picha hapo juu anaonekana Ridolf Elmer ambaye alikutwa na hatia ya kutoa nyaraka za siri za benki kwa mtandao wa habari wa Wikileaks. Jumuiya za nchi za kiarabu za tahadhalishwa.
Sharm el Sheikh, Misri-19/01/2011. Viongozi wa nchi za Kiarabu wamekutana nchini Misri ili kutasmini hali halisi ya jumuiya hiyo na kujadili wimbi la magauzi ambalo linaelekea kuzikumba nchi za Kiarabu.
Amir Mussa ambaye ni katibu mkuu wa jumuia ya nchi za Kiaarabu waliwaambia viongozi wa nchi wanachama ya kuwa hali ya kiuchumi katika nchi hizo inabidi ziangaliwe kwa undani sana, na "inatakiwa kuwepo na mabadiliko ya kiuchumi kwa serikali hizo kuwekeza rasilimali vitega uchumi ilikuinua maisha ya wanchi wa nchi hizo."
Akiongezea Amr Mussa alisema "mapinduzi yaliyo tokea nchini Tunisia lazima ma yaangaliwe kama mfano kwa serikali za nchi hizo."Na aliwataka wanchi wa nchi za Kiarabu kuwa pamoja ili kujenga nchi zao na eneo zima kwa ujumla.
Picha hapo juu anaonekana rais wa Misri Hosni Mubaraka akipokea ujumbe toka kwa moja ya washuri na huku katibu Amr Muoussa, akiangalia kwa makini.

No comments: