Wednesday, January 26, 2011

Uchumi wa dunia kujadiliwa tena Davos.

Uchumi wa dunia kujadiliwa tena Davos. Davos,Swiss - 26/01/2011. Viongozi wa serikali, wafanya biashara,,wanasiasa na wanauchumi, wanakutana nchi Uswisi ili kujadili mpangilio mzima wa uchumi dunia. Mkutano huo ambao utachukua siku tano, unatarajiwa kujadili mbinu za kuinua uchumi baada ya mtikiso mkubwa wa uchumi ulio ikumba dunia miaka miwili iliyo pita. Kwa mujibu wa wachunguzi wa maswala ya kiuchumi wanasema " inabidi katika mkutano huu viongozi, wanasiasa,wafanya biashara na wanauchumi watafute ufumbuzi wa kuinua uchumi na siyo kuweka ahadi ambazo zimekuwa ziki tawaliwa na mzunguko wa siasa na hai halisi ya kiuchumi. Picha hapo juu ni mji wa Davos, ambao viongozi wa nchi tofauti, wafanya biashara, wanasiasa na wanauchumi wanakutana kujadili hai halisi ya uchumi duniani.

Interpol yaombwa kumkamata rais wa Tunisia.
Tunis,Tunisia - 26/01/2011. Polisi wa kimataifa wameombwa kukamata aliye kuwa rais wa Tunisia, mkewe na washiriki wa karibu wa familia yake ili wajibu mashitaka mbele ya mahaakama.
Zine Kwa mujibu wa habari kutoka wizara ya sheria ya Tunisia zinasema "El Abidine Ben Ali, ambaye alikuwa rais wa Tunisi anakabiliwa na kesi za kuiba mali ya uma,kuiba pesa za nchi na kuziwekeza nje ya nchi kwa matumizi yake na familia yake."
Akisisitiza kuhusu habari hizo, Lazhar Karoui Chebbi, alisema tumeiomba Interpol kumkamata iliaje kujibu mashitaka ya kuhujumu mali umma.
Rais wa Tunisia alikimbia nchi baada ya wanchi wa Tunisia kuanamana kwa kutaka ajitoe madarakani kutona na serikali yake kushindwa kuwainua wanachi kiuchumi.
Umoja wa mataifa watakiwa kufungua mahakama za kiharamia.
New York, Amerika - 26/01/2011. Umoja a Mataaifa umeombwa kuchangia mbinu mbadala za kupambana na maharamia waliopo katika pwani ya Somalia hadi kufikia pwani za Afrika ya Mashariki na kuanzisha koti maarumu itakayo husika na kesi za kiaaramia.
Jack Lang, ambaye alikuwa waziri wa utamaduni wa Ufaransa, alisema " inabidi kuanzishwa koti ya kushughulkia kesi za kiaramia ili kukabili mlolongo wa watuhumiwa ambao huwa wanaachiwa huru.
Hadi kufikia sasa serikali ya Kenya na Ushelisheli ndizo zilizo weza kuwahukumu maharamia kwa kutumia sheria zilizpo nchini mwao.
Picha hapo juu wanaonekanaa baadhi ya maharamia wakinyoosha mikono mara baada ya kuwekwa chini ya ulinzi.

No comments: