Friday, January 28, 2011

Serikali ya Misri ipo njia panda.

Nelson Mandela aruhusiwa kutoka hospital. Main Image Johannesburg, Afrika ya Kusin - 28/01/2011. Aliyekuwa rais wa kwanza baada ya kuanguka kwa utawala wa kibaguzi wa makaburu ameruhusi kutoka hospital Mill Park ambako alikuwa amekwenda kwa matibabu. Nelson Mandela mwenye umri wa miaka 92 alikuwa hospitalini kwa matibabu baada ya kutojisikia vizuri kiafya. Makamu wa rais Kgalema Motlanthe aisema " Mandela ana nafuu na alikuwa anataniana nasi na tuzidi kumwombea afya yake iwe nzuri." Picha hapo juu anaonekana Winnie Mandela akitokea hospital kumwangalia mumewe Nelson Mandela ambaye alikuwa amelazwa hospital. Serikali ya Misri ipo njia panda. Kairo, Misri 28/01/2011.Maelfu ya wananchi nchini Misri wameandamana kupinga serikali iliyopo madarakani na huku polisi wakipambana na waandamaji kwa kutumia gasi na maji.

Kwa mujibu wa mashaihidi waliokuwemo kwenye maandamano walisema watu wengi wamejeruhiwa wakiwemo wakinamama.
Katika maandamano hayo alikuwemo aliyekuwa mkurugenzi wa shirika la kukagua na kumiliki mmatumizi ya nyuklia Mohamed ElBaradei.
Kufuatia maandamano hayo serikali imefunga matumizi yote ya mtandao, jambo ambalo jumuia ya kimataifa imelitilia mashaka kitendo hicho.
Picha hpo juu wanaonekana polisi wa kuzuia ghasia wakiwa wamesimama kuwazuia waandamanaji.

No comments: