Saturday, January 22, 2011

Tony Blair awelwa kiti moto tena.

Tony Blair awekwa kiti moto tena London, Uingereza - 22/01/2011. Aliyekuwa waziri mkuu wa Uingereza wakati wa vita vya Irak na kumtoa madarakani hayati Saadam Hussein ameojiwa kwa mara nyingine tena na tume ya uchunguzi wa mwenendo mzima wa vita vya Irak. Tony Blair ambaye alikuwa waziri mkuu wa Uingereza, chini ya serikali yake alishirikiana na serikali ya Amerika iliyo kuwa ikiongozwa na rais George Bush na kumn'goa madarakani rais Saadam Hussein wa Irak. Akiongea mbele ya tume hiyo Tony Blair alisema " nasikitika kwa kwa wale wote waliopoteza maisha au kuathirika kutokana na vita hivi." Na nilimwahidi rais wa Amerika ya kuwa kutakuwa bega kwa bega katika vita hivi kwani niliamini Saadam Hussein alikuwa kiongozi hatri kwa jumuia ya kimataifa." Uingereza na Amerika kwa kushirikiana na washiriki wengine ziliongoza vita vilivyo vikia kungólewa madarakani kwa rais wa Irak, Saadam Hussein. Picha hpo juu ni ya aliye kuwa waziri mkuu wa Uingereza Tony Blair ambaye aalikuwa akijibu maswali kutoka katika tume ya kuchunguza mwenendo mzima wa vita vya Irak.

Kiongozi wa Al Qaeda atishia Wafaransa.
Paris,Ufaransa - 22/01/2011. Kiongozi wa kundi la Al Qaeda ametishia na kuitaka serikali ya Ufaransa kutoa wanajeshi wake aliopo katika nchi za Kiislaam.
Osama Bin Laden alisema kwa kupitia habari zilizo patikana katika vyombo vya habarai kwa kudai " ili raia wa Ufaransa waachiwe inategemea uamuzi wa serikali yao kutimiza moja ya masharti ambapo ni kwa serikali ya Ufaransa kutoa majeshi yake katika nchi za Kiislaam."
Kuongea huko kwa kiongozi wa Kundi la Al Qaeda kunaendana na kuungwa mkono m\na na kundi la AQIM ambalo ndilo kundi kubwa lililopo Kaskazini Magharibi mwa Afrika linalo shirikiana na Al Qaeda, na hivi karibuni limehusika katika mauaji na utekaji nyara wa wengi raia wa Ufaransa.
Picha hpo juu ni ya Osama Bin Laden, ambaye ni kiongozi wa kundi la Al Qaeda, na hajulikani mahali alipo au anapo ishi.

No comments: