Friday, August 12, 2011

Katibu mkuu umoja wamataifa awa na wasiwasi juu ya wanchi wa Libya.

Uingereza yapata hasara ya mamilion kutokana na vurugu za uvunjaji.

London, Uingereza- 12/08/2011. Serikali ya Uingereza imekadilia uaharibifu uliyo fanywa wakati wa machafuko na uvunjaji ulio tokea hivi karibuni huenda ukafikia £100 million.
Hata hivyo waziri mkuu wa Uingereza David Cameron amehaidi ya kuwa serikali itawasaidia wale wote waliopata hasara kutokana na uvunjaji huo na kuhidi kwa kusema " serikali itafanya kila njia kuwakamata wale wote waliofanya vitendo hivyo ili waaadhibiwe kisheria."
"Na serikali itahakikisha inaweka mbinu mbadala ili kuzuia vitendo kama hivyo visitokee tena hapo baadaye." Alimalizia waziri mkuu David Cameron.
Hadi kufikia sasa zaidi ya watu 900 wameshakamatwa kwa kuhusika na machafuko hayo ambayo yame wame wapa mashaka wakazi wa Uingereza.
Katibu mkuu aumoja wa mataifa awa na wasiwasi juu ya wanchi wa Libya.
New York, Marekani - 12/08/2011. Msemaji wa katibu mkuu wa umoja wa mataifa amelezea wasiwasi alionao katibu mkuu,kufuatia ripoti ya kuwa raia wa kawaida wamekuwa wakipoteza maisha kwenye vita vinavyo endelea nchini Libya.
Msemaji huyo alisema, katibu mkuu amezitaka pande zote mbili zinazo pigana chini humo kutafuta suruhisho lili kusimamisha umwagaji wa damu.
Nayo serikali ya Libya imelilaumu jeshi la NATO kwa kushanmbulia maeneo ya raia kila inapo fanya mashambulizi yake.
Hata hivyo jeshi la NATO limesema " huwa linafanya mashambulizi kwenye kambi za majeshi ya Libya na siyo maeneo ya raia.

No comments: