Sunday, August 28, 2011

Mapadri wazidi kujitoa katika Kanisa Katholiki nchini Kenya ili kuoa.

Al Qaeda namba mbili auwawa.
Islambad, Pakistan - 28/02/2011.Kiongozi wapili kimadaraka katika kundi la Al Qaeda ameuwawa nchini Pakistani.
Atiya Abdul Rahman raia wa Libya ambaye inaaminika alikuwa muhimu katika kupanga mbinu zote za mashambulizi la kundi la Al Qaeda na alikuwa anawasiliana moja kwa moja Osama Bin Laden ambaye aliuwawa miezi michache iliyopita.
Kifo cha Atiya Abdul Rahman, kinasadikiwa ni pigo kubwa kwa kundi hilo, kwani ndiye mtu ambaye alikuwa "anaweza kumsaidia kiongozi wa sasa wa Al Qaeda Ayman al Zawahiri katika kuimarisha kundi hilo."
Kifo chake kimetokea baada ya ndege ya kijeshi inayo endeshwa na ongozwa na mtandao kushambulia eneo alilo kuwa amejificha.
Kundi la Al Qaeda lina ongozwa na Ayman al Zawahiri,baada ya kifo cha kiongozi wa kundi hilo Osama bin Laden.
Mapadri wazidi kujitoa katika Kanisa Katholiki nchini Kenya ili kuoa.
Nairobi, Kenya - 28/08/2011. Zaidi ya mapadri 40 wameamu kujitoa katika kanisa Katoliki na kujiunga na Kanisa la Ekumenikal Katholik ili waweza kuoa na kuwa nafamilia kwa kipindi cha miaka miwili iliyopita.
Askofu wa Kanisa la Ekumenikal Katholik, Geoffrey Shiundu, ambaye alijitoa katika kanisa mama la Katholik baada ya kuamua kuoa, alisema "kanisa la Ekumenikal linazidi kukua na mapadri wanadizi kujiunga nalo."
"Tutaweza kushirikiana na kanisa mama la Katholik kama Papa Benedikt XVI atakubali kubadili muundo wa kanisa kwa kuweka huru, ikiwa padri anataka kuoa aoe na kama hataki basi abaki bila kuoa." Alisisitiza.
Askofu Shiundu aliyasema hayo wakati wa sherehe ya kumweka wakfu mmoja wa mapadri kwenye mji wa Kitale.
Libya yarudishiwa uanachama na jumuiya ya nchi za Kiarabu.
Kairo
,Misri - 28/07/2011. Shirikisho la nchi za jumuiya ya Kiarabu remeirudishia uanachama wake Libya baada yakuangushwa kwa utawala wa Muammar Gaddafi.
Msemaji wa jumuiya hiyo Nabil Elarab alisema " bendela mpya ya serikali ya mmpito itawekwa na ile ya serikali ya Muammar Gaddafi ambayo ilikuwa na rangi ya kijani itatolewa."
Libya ilitolewa katika jumuiya hiyo baada ya serikali ya Muammar Gaddafi kuanza kupambana na wapinzani waliokuwa wanaipinga serikali yake mapema mwezi wa pili mwaka huu.

No comments: