China na Marekani zakutana kujadili mabadiliko uchumi.

Beijing, China 18/08/2011. Serikali za China na Marekani zimekubaliana kuendelea kufanya biashara ingawa kuna baadhi ya vikwazo ambavyo vipo kati ya nchi mbili hizo.
Makamu wa rais wa China akimkaribisha mgeni, wake makamu wa rais wa Marekani Joe Biden,ambaye yupo ziarani nchini China, Xi Jinping alisema "Marekani ni nchi ambayo inatakiwa kuimarika kiuchumi,kwani uchumi wake ni kiungo cha duniani."
Makamu wa rais Joe Biden yupo nchini China ilikujadili maswala ya kiuchumi na biashara na serakali ya China .
Hata hivyo habari kutoka serikali ya China zinasema, makamu wa rais Xi Jinping atazungumzia swala la Marekani kutaka kuuzia Taiwani zana za kijeshi.
Rais wa zamani wa Ivory Coast afunguliwa mashitaka.

Laurent Gbagbo, ambaye alitolewa madarani kwa nguvu na jeshi la rais wa sasa Alassane Outtara, anakabiliwa kujibu mashitaka ya kutumia fedha na mali za serikali kabla na baada ya uchaguzi kwa manufaa ya kumsaidia kubaki madarakani.
Hata hivyo wasemaji wa kutetea haki za binadamu, hawakulizika na kesi hiyo kwa madai ni "haina uzito kulinganisha na mauaji na uharibifu uliyo tokea wakati wa vita kati ya wanajeshi wa Gbagbo na Outtara mara ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa baaada ya Laurent Gbagbo kudai yakuwa yeye ndiye alishinda uchaguzi.
No comments:
Post a Comment