Serikali ya Kenya yakasirishwa na Luis Moreno Ocampo.

Nairobi, Kenya - 22/08/2011. Serikali ya Kenya imekasirishwa na kitendo cha mwanasheria mkuu wa mahakama ya makosa ya jinai iliyopo nchini Uhollanzi, kwa kuihusisha ikulu katika machafuko ya kisiasa yaliyo tokea nchini humo.
Habari kutoka ikulu zinasema, "ofisi ya rais imekasirishwa sana na Luis Moreno Ocampo kuwahusisha wafanya kazi wa karibu wa rais Mwai Kibaki katika machafuko ya kisiasa."
Hata hivyo habari kutoka ofisi ya Luis Moreno Ocampo zinasema " ripoti hiyo haikuwahusisha rais na waziri mkuu wa Kenya."
Ripoti hiyo ya Luis Moreno Ocampo imekuja baada ya uchunguzi uliyo fanywa na ofisi yake nchini Kenya, baada ya machafuko yaliyo leta hasara kwa raia na mamia kupoteza misha kabla na baada ya uchaguzi mkuu uliyofanyika nchini humo mwaka 2007 .
Wamarekani wahukumiwa kwenda jela nchini Iran.

Watuhumiwa hao, Josh Fattal na Shane Bauer walihukumiwa kwenda jela miaka minane kila mmoja, baada ya ya mahakama kuwakuta na hatia na kuamua kuwahukumu miaka mitano kila mmoja kwa kosa la kufanya ukachelo na miaka mitatu kila mmoja kwa kosa la kuingia nchini Iran kinyume cha sheria.
Mwanasheria anaye wawakilisha wa Marekani hao alisema " natumani wateja wangu wataachiwa kwa msamaaha wa serikali, baada ya wazazi wa watuhumiwa hao kuiomba serikali ya Iran kuwaachia kwa kuzingatia ni mwezi mtukufu wa Ramdhani, kwani hawakufanya makosa yoyote"
Josh na Shane walikamatwa 31/Julai/2009 baada ya serikali ya Iran kudai walikuwa wamevuka mpaka na kuingia nchini humo kutokea eneo la Kikurdish lililopo nchini Irak.
No comments:
Post a Comment