Serikali ya Marekani kukabiliana na maafa ya Irine.


Washington, Marekani - 29/08/2011. Kimbunga na mafuriko ambacho kimetokea nchini Marekani kimesababisha uaribifu mkubwa na kupoteza maisha ya watu kwa mujibu serikali.
Mafuriko hayo na kimbunga ambacho kilianza wiki iliyopita yamesababisha nyumba na barabara kubomoka na kufanya hali ya maisha na mawasiliano kuwa ngumu.
Craig Fugate mkurugenzi mkuu wa maswala ya maafa alisema" serikali ina kibarua kigumu na itajitahidi kuwasaidia wale wote waliokumbwa na kumbunga Irine na kiasi cha mamillioni ya dola zinahitajika haraka sana ili kuanza kutoa huduma."
Kimbunga na mafuriko yaliyo sababishwa na Irine kimefuatia kimbunga Katalina kilicho sababisha maafama makubwa miaka michache iliyopita nchini Marekani.
Mbu wa malaria waelekea kupungua nchini Tanzania.

Dar es Salaam, Tanzania - 29/08/2011. Watafiti wa malaria nchini Tanzania wamedai yakuwa mbu ambao wanasababisha ugonjwa wa malaria wanaelekea kupungua.
Wanasayansi wa Tanzania na Denmarki wamegundua upunguaji wa mbu hao baada ya kufatilia idadi ya mbu ambao walikuwa wanapatikana na viini vya ugonjwa huo.
Profesa Dan Meyrowisch, alisema " upunguaji wa mbu hao ni kitu ambacho kinatakiwa kufanyiwa uchunguzi zaidi, ingawa inaweza sababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa na ukame."
Mpango wa kupambana na malaria umekuwa ikipewa kipao mbele ili kutokomeza malaria katika bara la Afrika ugonjwa ambao umekuwa unasababisha vifo vingi hasa kwa watoto wadogo.
Mshukiwa wa ulipuaji wa ndege ya Pan am jet anahali mbaya kuliko ilivyo zaniwa.

Tripol, Libya 29/08/2011. Mshukiwa ambaye inasadikiwa alihusika katika ajali ya ndege Pan Am Jet amekuwa na hali mbaya kiafya kuliko ilivyozaniwa na viongozi na wanasiasa wa Uingereza na Marekani.
Mohmed al Megrahi, ambaye aliachiwa huru mwaka 2009 na serikali ya Scotland na kurudi nchini mwake Libya baada ya kujilikana ya kuwa ana ugonjwa wa saratani- kansa ambayo itamfanya kutokuishi kwa muda mrefu.
Kuruhusiwa kwa Al Mergahi kumeleta mvutano kati ya wanasiasa na viongozi wa Uingereza na Marekani kwsa wengine kudai yakuwa arudishwe nchini Scotland kuendelea na kifungo.
Khaked al Megrahi, mtoto wa Mohmed Megrahi amesema " baba yangu ni mgojwa sana nahakuna mganga wala muhudumu ambaye tunawasiliana naye na hakuna msaada wowote tunapata, baba anatumia oksijeni na dawa zake zimekwisha hivyo tupo naye na hatujui nini la kufanya."
Waziri wa sheria wa serikali ya mpito Mohamed al Alagi alisema, hakuna Mlibya yoyote atakaye pelekwa nchi za magharibi ili kujibu mashitaka, hivyo Mohmed al Megrahi atapelekwa kokote."
Nayo serikali ya Scotland imesema " alifanya jambo la kiutu na Mohmed al Magrahi hatarudishwa nchini, na ushahidi umeonyesha yakuwa tulivyo amua kumuachia kwani hali yake sasa siyo nzuri."
Mashariki ya Uganda yakumbwa na maporomoko.

Msemaji wa shirika la msalaba mwekundu Catherin Ntabade alisema " mvua kubwa iliyonyesha ndiyo iliyo sababisha maporokomo hayo na hadi sasa watu wapatao 23 wamepoteza maisha na watu wengine hawajulikani wapo wapi."
Serikali ya Uganda imepeleka kikosi cha waokoaji na misaada mingine ili kukabiliana na tukio hilo.
Maporooko kama haya yalitokea mwaka jana kwenye eneo karibu na mlima Elgon kwenye mpaka wa Kenya na Uganda na kuleta maafa makubwa kwa jamii na mazingira.
No comments:
Post a Comment