Kesi zidi ya Dominik-Strauss Kahn yafutwa na aachiwa huru.

Jaji Michel Obus aliamua kufuta kesi hiyo baada ya mwanasheria kwa upande wa mashitaka kudai ya kuwa "kesi zidi ya Dominik Strauss-Kahn haina ushaidi wa kutosha kwa kuzingatia ukweli wa bi Diallo ambao ameusema alipo wasili nchini Marekani."
Mwanasheria Kenneth Thompson ambaye anamtete mshitaki alisema" mwanasheria wa serikali ameamua kutokubaliana na haki ya mwanamke asiyekuwa na makosa kuweza kupata haki yake kutokana mambo yaliyomtokea."
Baada ya uamuzi wa mahakama kufuta kesi, familia ya Strauss-Kahn ilisema " kipindi chote cha kesi hii familia yetu ilikuwa aina furaha na kuanzia sasa tunaweza kuanza upya maisha ya kujenga familia yetu ."
Kufuatia uamuzi wa mahaka kufuta kesi, Dominik Strauss-Kahn yupo huru na anaweza kusafiri kurudi nchini kwake Ufaransa.
Dominik Strauss-Kahn alifunguliwa mashitaka baada mfanyakazi katika hotel aliyo kuwa amefikia kufungua kesi ya ubakwaji zidi yake.
No comments:
Post a Comment