Tuesday, August 23, 2011

Vita vya LIbya vyaingia sura mpya na Saif al Islaam yupo huru.

Afrika ya Kusini na Burundi zasahini mikataba ya kiuchumi.
Bujumbura, Burundi -23/08/2011. Serikali za Afrika ya Kusini na Burundi zimetiliana sahii mikataba ya kiuchumi kati ya nchi hizo ili kuimarisha maendeleo na kukuza ukaribu zaidi
Mikataba hiyo ilisainiwa wakati rais wa Afrika ya Kusini, Jakob Zuma alipo fanya ziara ya kiserikali nchini Burundi, ili kudumisha ushirikiano uliopo kati ya nchi hizo mbili, na kwa kuzingatia rais Jacob Zuma alikuwa mmoja wa wasuruhishi katika jitihada za kuleta amani nchini Burundi.
Katika mikataba hiyo nchini hizo zitashirikiana katika sekta za kilimo,usafiri na kifedha, ambapo kutaongezea nguvu kiuchumi hasa kwa nchi ya Burundi ambayo ilikumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa muda mrefu hadi vilipo kwisha hivi miaka ya karibuni.
Vita vya Libya vyaingia sura mpya na Saif al Islaam yupo huru.
Tripoli
, Libya - 23/08/2011.Mtoto wa kiume wa kiongozi wa Libya ameonekana na kuongea na waandishi wa habari, masaaa machache baada ya kundi la upinzani kutangaza yakuwa wame mkamata yeye na ndugu zake.
Huku akishangiliwa na wadau na wale wanao muunga mkono baba yake, Saif al-Islaam alisema " mimi nipo na kundi la wapinzani limekwisha na utiwake wa mgongo umesha uvunja. Na baba yangu yupo salama na tutashinda zidi yawale wanaotaka mali ya Libya."
Pia alimalizia kwa kusema" kesi zidi ya mahakama ya kimataifa ya Uhollanzi hainisumbui kichwa na kwasasa kundi la upinzani limekwisha na jiji la Tripol lipo chini ya mikono yetu."
Kufuatia kuoneana kwa Saif al Islaam, viongozi wa kimataifa wamekuwa wakitoa maelezo tofauti na kusisitiza yakuwa muda si mrefu utawala wa Muammar Gaddafi utaporomoka na Libya itakuwa huru.
Saif al Islaam ambaye alizaniwa kuchukua madaraka ya baba yake, amekuwa ndiye msemaji mkuu wa serikali ya baba yake na kuhaidi yakuwa serikali ya baba yake itashinda.

No comments: