Waumini wa dini ya Kislaam washerekea kumaliza mwezi wa Ramadhani.

Makka, Saud Arabia 31/08/2011. Waumini wa dini ya Kislaam duniani wamesherekea sikukuu ya Iddi baada ya kumaliza mwezi wa Ramadhani.
Sikukuu ya Iddi huwa inasherekewa na waumini wa dini ya Kislaam kwa kumaliza mwezi Ramadhani baada kufunga -kwa kujizuia kula kwa kipindi chote cha mwezi mzima ikiwa njia ya kuomba toba.
Mwezi huu wa Ramadhani, waumini wa dini ya Kislaam, huwa wanaamini ya kuwa nikipindi cha kufanya mema na kutafakali yale yote waliyo yafanya na pia kumwomba "Mungu awasamehe zambi kwa huruma yake." Pia kuangali ni kwa kiasi gani watajitahidi kufanya mazuri zaidi katika maisha yanayo fuata.

Sedney, Australia - 31/08/2011. Mahakama kuu nchini Australia imezuia amri ya serikali ya kutaka kubadilishana wakimbizi waliopo nchini humo na wakimbizi waliopo nchini Malaysia.
Uamuzi huo wa mahakama umekuja baada ya serikali ya Australia na Malaysia kukubaliana kubadilishana wakimbizi mapema mwezi May mwaka huu.
Makubaliano hayo yalikuja wakati mawaziri wakuu wa nchi hizo walipokutana na kujadili mbinu za kuzuia biashara ya kusafirisha watu kati ya nchi hizo.
Katika kutoa hukumu hiyo, mahakama ilisema "Malaysia siyo nchi mwanachama katika makubaliano ya maswala ya ukimbizi ya mwaka 1959 chini ya umoja wa mataifa na hivyo wakimbizi wanatakiwa wapewe haki sawa kwa kufatia sheria za kimataifa na zakitaifa."
1 comment:
Simply wish to say your article is as amazing. The clarity in your post is just nice and i can assume you're an expert on this subject. Well with your permission allow me to grab your RSS feed to keep updated with forthcoming post. Thanks a million and please keep up the gratifying work.
Feel free to visit my web site ... tazmanian
Post a Comment