Rwanda na Uganda kuimarisha ushirikiano uliyopo.

Kigali,Rwanda - 02/08/2011. Marais wa Rwanda na Uganda wamehaidi kuimarisha uhusiano uliyopo kwa ajli ya wananchi wa nchi hizo na jumuiya nzima ya Afrika Mashariki.
Marais hao Paul Kagame na Yoweri Museven waliyaongea haya wakati walipo kutaka kwenye chakula cha jioni kilichoandaliwa na mke wa rais Paul Kagame.
Rais Yoweri Museven alifanya ziara nchini Rwanda ili kudumisha uhusiano na nchi hiyo kwa ukaribu na kujadili mikakati ya kuimarisha jumuiya ya Afrika Mashariki.
Hugo Chavez amuunga mkono Muammar Gaddafi.

Karakas, Venezuela - 02/08/2011. Rais wa Venezuela ameliambia taifa ya kuwa amepokea barua kutoka kwa rafiki yake mwanamapinduzi kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi.
Rais, Hugo Charez alisema " nimeisoma barua hiyo na kuilewa na nitaendelea kumuunga mkono kiongozi mwana mapinduzi Muammar Gaddafi ambaye anapigania haki ya wanchi wake na nakutakia maisha marefu Muammar Gaddafi."
"Nawale note ambao wanamwaunga mkono wapinzani wa Gaddafi hawajui nimakosa wamefanya."
Rais Hugo Chavez ambaye alikuwa amenyoa nywele, aliyaema haya wakati alipo kutana na waandishi wa habari mara baada ya kuwasili kutoka nchi Kuba kwa matibabu ya kansa.
Na habari kutoka nchi Libya zinasema kiongozi wa nchi hiyo Muammar Gaddafi amemshukuru rais wa Venezuela kwa kuwanaye pamoja wakati wa shida na ameonyesha ni rafiki wa kweli."
Iraka yatakiwa kufanya uamuzi wa haraka kuhusu jeshi la Marekani.

Admiral Mike Mullen alisema " inawabidi viongozi wa Irak kuamua kama wanataka jeshi la Amerika liendelee kuwepo nchini humo baada ya Desemba 31 kwani muda unakwenda haraka."
"Na inabidi wanajeshi wa Amerika wapewe huakika wa kisheria ikiwa wataiendelea kuwepo nchini Irak" alisema Admiral Mike Mullen.
Hata hivyo habari kutoka serikali ya Irak zinamsema " viongozi wa serikali ya Irak wapo na wakati mgumu hasa kutoka kwa wanachi wanchi hiyo na jumuiya ya kimataifa kutokana na hali halisi iliyopo nchini humo, hasa katika swala zima la usalama."
Marekani bado inawanajeshi wapatao 46,000 ambao bado wanaendelea na kazi ya kulisaidia jeshi la Irak katika maswala ya ulinzi.
No comments:
Post a Comment