Thursday, August 25, 2011

Zawadi nono kutolewa kwa atakaye toa habari alipo Gaddafi akiwa mzima au amekufa.

Jean-Pierre Bemba kugombea urais wa Kongo DR.
Kinshasa, Kongo DR - 25/08/2011. Kiongozi wa chama cha upinzani nchini Kongo, naambaye yupo chini ya mahakama ya kimataifa ya kuzuia hualifu amehaidi kugombea kiti cha urais katika uchaguzi unao tarajiwa kufanyika mwisho wa mwaka 2011.
Jean Pierre Bemba ambaye ni kiongozi wa chama- MLC, Movement Liberation of Congo amesema hayo kupitia mwanasheria wake Aime Kilolo ya kuwa "atagombani kiti cha urais ijapokuwa yupo na kesi."
Memba ambaye alikamatwa 2008 nchini Uberigiji na kufunguliwa kesi ya kukiuka haki za binadamu kwenye mahakama ya kutetea haki za binadamu iliyopo Hague nchini Uhollanzi wakati wa jeshi lake lilipo kuwa linapambana na jeshi la serikali kati ya mwaka 2002 na 2003
Habari zilizo patikana zinamsema akiwa kizuizini Jean Pierre Bemba ameweza kutana na wakongo wengi wakiwemo viongozi wa upinzani Etiene Tshisekedi, Vital Kamerhe na Leon Kengowa Dondo.
Zawadi nono kutolewa kwa atakaye toa habari alipo Gaddafi akiwa mzima au amekufa.
Benghazi,
Libya -25/08/2011. Serikali ya mpito ambayo inapambana katika kuing'oa madarakani serikali ya Libya imetangaza kutoa zawadi ya fedha kwa mtu yoyote atakaye toa habari wapi yupo kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi ili akamtwe akiwa mzima au amekufa.
Guma el Gamaty ambaye ni mmoja wa viongozi wa serikali ya mpito, alisema " hii ni nafasi ya dhahabu ya $ 1.7million zitatolewa ikiwa mtu yoyote atatoa habari za kupatikana kwa Muammar Gaddafi"
Zawadi hii imetolewa na wafanya biashara kwa kusaidia na serikali ya mpito ambayo wapiganaji wake wanapigana na serikali ya Muammar Gaddafi.
Nayo serikali ya Itali imekubali kuachilia pesa za zilizo kuwa za serikali ya Muammar gaddafi ili kusaidia serikali ya mpito.
Hadi sasa Muammar Gaddafi na familia yake hawajulikani wapo wapi, baada ya kundi la upinzani kuingia katika jiji la Tripoli hivi karibuni.

No comments: