Monday, September 12, 2011

Watanzania waanza maombelezi baada ya ajali ya boti.

Bomba la mafuta la lipuka nchini Kenya na kuleta maafa makubwa.
Nairobi, Kenya - 12/09/2011.Watu 63 wamepoteza maisha yao na wengine zaidi ya 110 kijeruhiwa vibaya baada bomba la mafuta kupasuka na kuanza kuvuja na baadaye kuwaka moto katika eneo la viwanda la Lunga Lunga.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema "inaminika moto huo umetokea baada ya kipande cha sigara kudondoka katika moja ya tundu kikilopo kwenye bomba hilo."
Msemaji wa polisi Erick Kiraithe alisema " huenda vifo vikaongezeka kutokana ajali hiyo."
Bomba hilo ambalo limepita katika maeneo anayo kaliwa na watu , lili kuwa lina vuja na kuwafanya wakazi wa maeneo hayo kwenda kukinga mafuta, jambo ambao limesababisha watu wengi kujeruhiwa na wengine kupoteza maisha baada ya mafuta hayo kushika moto na kulipuka.
Watanzania waanza maombolezi baada ya ajali ya boti Unguja.
Unguja, Zanzibar -12/09/2011. Wananchi wa kisiwa cha Zanzibar na Tanzania kwa ujumla wamenza maombelezi kwa muda wa siku tatu baada ya ajali ya boti iliyo kuwa imebeba abiria kuelekea Pemba kuzama na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 200.
Boti hiyo ambayo ilikuwa imebeba watu wapatao 800 na mizigo kwa kiasi kingi, ilizama kilomita chache baada ya kutoka bandari ya Unguja.
Kwa mujibu wa habari zina sema "boti hiyo ilikuwa na uwezo wa kuchukuwa watu 600, lakini ilikuwa imelizidisha watu pamoja na mizigo kabla ya kuondoka na kufanya baadhi ya abiria kuamua kushuka kutokana na wingi wa watu.
Mmoja wa abiria waliokuwemo kwenye boti hiyo Yahya Hussein alisema " nilihisi kuna matatizo baada ya kuanza kuona meli inakwenda alijojo na mwendo wa kuyumba na nikaona bora niliruke wakati meli inaanza kuzama na shukuru ubao nilioshikilia ndoyo uliyo niokoa nisizame."
Nayo serikali ya Tanzania imeunda tume ya uchunguzi kuchunguza chanzo cha ajali hiyo na vile vile kutoa misaada ya kifedha na mali ili kuwafariji waliopotelewa na ndugu na jamaa zao kutokana na ajali hiyo.
Baraka Obama na George Bush waudhuria siku ya kumbukumbu ya Sept/11.
, Marekani - 12/09/2011. Rais Baraka Omaba wa Marekani amewaongoza wananchi katika maombelezi ya kuadhimisha miaka 10 tangu kufanywa kwa mashambulizi ya kigaidi jijini New York.
Baraka Obama alisema "hakuna kitu kitautikisa au kubomboa umoja wa Wamarekani na daima tutakuwa pamoja."
"Na tutapambana na ugaidi hadi tuutokomeze, na tutazidi kuwakumbuka wale wote waliopoteza maisha yao katika kulitetea taifa letu na kuenzi yote waliotufanyia.
Sherehe za kumbukumbu za kuwakumbuka wale wote waliopoteza maisha yao kutokana na mashambulizi yaliyofanywa kwenye majengo ya marefu yaliyo kuwa katikati ya jiji la New York ambapo zaidi ya watu 2900 waliuwawa na magaidi kwa kushirikiana na kundi la Al Qaeda na kuharibu malizingira ya jiji hilo, ziliudhuriwa pia na aliyekuwa rais wakati wa mashambulizi hayo George Bush na viongozi wengine wa serikali.

No comments: