Thursday, September 29, 2011

Ujerumani yaingeza nguvu sarafu ya Euro.

Mahakama kuendelea kusikiliza kesi kuhusu kifo cha Michael Jackson.

Los Angeles, Marekani -29/09/2011. Mahakama katika jiji la Los Angeles, bado inaendelea kusikiliza kesi zidi ya mganga Conrad Murrey, ambaye anashutumiwa kwa kosa la kusababisha kifo cha nyota na bingwa wa musiki ya pop Michael Jackson.
Kesi hiyo ambayo imeanza hivi karibuni, baada ya uchunguzi kumalizika ili kujua nini kilimwua bingwa huo wa musiki
Hata hivyo muuguzi huo Conrad Murray amekana kosa hilo na kesi bado inaendelea kusikilizwa.
Ujerumani yaiongeza nguvu ya sarafu ya Euro.
Berlin, Ujerumani-29/09/2011.Bunge la Ujerumani limeidhini kwa kura mswada wa serikali ya nchi hiyo kuikomboa sarafu ya euro ambayo ilikuwa ipo mashakani kutoka na myumbo wa kiuchumi fedha uliyopo katika nchi wanachama wa jumuia ya Ulaya.
Matokeo ya kura 523 yaliyo unga mkono muswada huo, yalimpa uhai mkubwa Kansela Angela Merkel, kwani hapo mwanzo wa majadiliano ya muswada huo ilionekana ya kuwa itakuwa vigumu kupitishwa.
Kufuatia uamuzi huo wa Ujerumani kuilinda sarafu ya euro, masoko ya fedha katika bara la ulaya yalionekana kufanya vizuri kwa hisa kupanda.
Ujerumani imekuwa nchi pekee katika nchi wananchama wa jumuia ya Ulaya ambayo imekuwa inasimamia sarafu ya eoro kwa hali na mali.
Waganga na wauguzi wahukumiwa kwenda jela Bahrain.
Manama, Bahrain - 29/09/2011.Maganga na wauguzi ambao walishiriki kuwatibu watu walioumia wakati wa maandamano ya kupinga serikali wamehukumiwa vifungo vya miaka tofauti kati miaka 5 na 15 jela.
Waganga hao na wauguzi ambao walikuwa katika hospitali ya Sulmania, wanashutumiwa kuwa kwa kuwatishia walinzi wa usalama kwa kutumia siraha, visu na vifaa vingine vya kufanyia upasuaji.
Msemaji wa wizara ya habari ya Bahrain Sheikh Mubarak Abdulaziz Khalifa alisema "waganga hao na wauguzi walifanya kitendo cha kigaidi kwa kuwazuia walinzi wa usalama wasifanye kazi zao na kushiriki katika maandano kinyume na sheria."
Hata hivyo wauguzi hao walikana makosa hayo na kuomba shirikisho la wauguzi kuingilia dunia kuingilia jambo hili kwa kudai "nikinyume na sheria za uuguzi."
Mpinzani wa serikali ya Bahrain Matar Matar alisema " serikali ainatakiwa kutatua matatizo yaliyopo na hasa ya kisiasa kwani ndiyo chanzo cha kutoluwa na amani."

No comments: