Tuesday, September 27, 2011

Mshindi wa Nobel ya Laureate mama Wangari Mathai hatuko naye tena.

Mshindi wa Nobel ya Laureate mama Wangari Mathai hatuko naye tena.

Nairobi, Kenya 27/09/2011. Wananchi wa Kenya wamkutwa na msiba baada ya kuondokewa na aliyekuwa mtetezi na mwanzilishi wa kitengo cha kuboresha mazingira nchini humo kinacho julikana kama Green Belt Movement Bi Wangari Mathai.
Wangari Mathai ambaye alikuwa mwanamke wa kwanza kutoka Afrika kutunikiwa nishani ya Nobel Laureate, alifariki dunia kutokana na ugonjwa wa saratani katika hospital jijini Nairobi.
Msemaji wa familia ya Bi Mathai alisema " tumepata masikitiko makubwa na majonzi kwa kuondokewa na mama yetu mpendwa, ndugu yetu, na mpenda haki."
Bi Wangari Mathai atakumbukwa kwa kuongoza maandamano ya kupinga serikali ya Kenya kutaka kuongeza mawaziri na pia kuwa mfano bora kwa wanawake wote wa Afrika katika kupigania haki, pia na kuongoza katika nyazifa mbalimbali serikalini ikiwemo uwaziri.