Thursday, September 1, 2011

Kenya hawatakuwa wanavaa nywele za bandia kwenye mahakama.

Kesi zidi ya machafuko ya Kenya yaanzwa kusikilizwa.
Hague, Uhollanzi -01/09/2011.Mahakama ya kimataifa inayoshughulikia kesi ya ukiukwaji wa haki za biadamu imeanza kusikiliza kesi zidi ya viongozi wanaoshutumiwa kuhusika na mauaji na machafuko yaliyo tokea nchini Kenya mwaka 2007 baada ya uchaguzi.
Washitakiwa hao ni waziri wa elimu William Ruto na ambaye alikuwa natarajiwa kugombea kiti cha urais katika uchaguzi ujao nchini Kenya.
Katika kesi hiyo " jaji wa mahakama hiyo alisema kesi hizo zidi ya washukiwa hao ipo kwa kusikilizwa na kuwapa nafasi washutumiwa kujitetea."
Kwa mujibu wa habari kutoka kwa washitakiwa wanasema" hatuna wasiwasi na ukweli utaonekana kama hatna makosa."
Kesi zidi ya Ruto na wenzake inatarajiwa kuchukua muda kabla ya hukumu kutolewa.
Kenya hawatakuwa wanavaa nywele za bandia kwenye mahakama.
Nairobi, Kenya 01/09/2011. Majaji nchini Kenya hawatakuwa wanatumia maneno ya "my lord or my lady" katika mahakama nchini huma, baada ya madiliko kufanywa katika wizara ya sheria hivi karibuni.
Jaji mkuu Willy Mutunga alisema " kuanzia sasa majaji watakuwa wanatumia maneno ya Muheshimiwa or your honour na hii ndi itakuwa lugha ya mawasiliano kati ya wana sheria na mahakama na hawataruhusiwa kuvaa nywele nyeupe za bandia kichwani na vilevile kutakuwa na vazi rasmi la kuvaa wakati wa kuendesha kesi kotini."
Uamuzi huo umekuja baada ya majaji na wanasheria kutaka mabadiliko ya kisheria na mazingira ya koti yabadilishwe.
Ugonjwa wa mafua ya ndege na kuku kutishia afya za watu tena.
Geneva, Uswisi - 01/09/2011. Shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia maswala ya kilomo na chakula (FAO) limeonya kuenea kwa ugonjwa wa mafua ya ndege na kuku.
Habari zinasema "ugonjwa wa mafua ya ndege na kuku (H5N1 unaelekea kusambaa nchini China na Vietnam na huenda ukafika Kambodia na nchi zilizopo kwenye ukanda wa Peninsula.
Ugojwa wa mafua ya kuku na ndege ni ugonjwa ambao una madhara katika jamii na umesha poteza maisha ya watu karibu kila sehemu duniani.
Sarkozy na Cameron wasimia mkutano wa Libya nchini Ufaransa.
Paris. Ufaransa - 01/09/2011. Mataifa sitini yanakutana nchini Ufaransa ili kujadili ujenzi na mipango ya kuijenga upya nchi ya Libya ambayo uchumi wake umeharibika kutokana na vita katika harakati za kung'oa madarakani Muammar Gaddafi.
Mkutano huo ambao umeitishwa na rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy na waziri mkuu wa Uingereza David Cameron, unatarajiwa kuitambua rasmi serikali ya mpito na kujadili njia ya kuwasaidia wa Libya ili kuinua uchumi wao.
Mustafa Abdel Jalil mwenyekiti wa serikali ya mpito alisema " tutaweka wazi muswada wetu wa kuunda katiba mpya na kujiandaa na uchaguzi baada ya miezi 18."
Habari kutoka kwenye mkutano huo zinasema " mkutano huo utakuwa wa hali ya juu, kwani nchi ambazo zilisaidia katika harakati za kumng'oa Muammar Gaddafi madarakani zitakuwa na wakati mgumu katika kujaribu kuweka masrahi yao mbele, hasa baada ya serikali ya mpito kusema zile nchi zilizo saidia katika mapinduzi zitapata malipo bora."
Mkutano huo wa Paris unafanyika wakati Muammar Gaddafi ametangaza tene kupitia TV na radio za nchini Syria ya kuwa atapambana hadi kufa na kuwataka wale wanao muunga mkono kupigana hadi mwisho.

No comments: