Tuesday, September 27, 2011

Serikali ya mpito ya Libya kutoendelea na kesi ya mtuhumiwa wa ajali ya ndege Pan Am 103.

Serikali ya mpito ya Libya kutoendelea na kesi ya mtuhumiwa wa ajali ya ndege Pan Am 103.

Tripol, Libya - 27//09/2011. Waziri wa sheria wa serikali ya mpito ya Libya ametangaza ya kuwa kesi zidi ya aliyekuwa mtuhumiwa katika kesi ya kulipuliwa ndege ya Pan Am 103 iliyo tokea Lockerbie haitaendelea na imefungwa.
Waziri Mohammed al-Alagi alisema " Abdel Basset al-Megrahi alisha hukumiwa na kuachiwa na koti kutokana na hali yake kwa makubaliano ya serikali za Skotilandi na Britishi, hivyo hawezi kushitakiwa marambili kutokana na kosa hilo."
Al Megrahi alikutwa na hatia ya kuhusika katika kulipua ndege ya Pan Am 103 liyokuwa imebeba watu 250 na kuhukumiwa mwaka 2001 kwa kosa la kusababisha vifo vya watu 260 kati yao 11 walikuwawa baada ya ndege kudondoka katika eneo walilo kuwepo.
Kuchiwa kwa Abdel Basset al-Megrahi kulileta mvutano mkubwa kati ya serikali za Uingereza, Marekani na ndugu wa raia walio uwawa katika ajali hiyo.
Iran na Sudan zazidi kudumisha uhusiano kwa ukaribu zaidi.
Khartoum, Sudan - 27/09/2011. Rais wa Iran yupo ziara nchini Sudan, ili kudumisha uhusiano uliyopo kati ya Iran na Sudan.
Katika ziara hiyo, rais wa Iran Mahamoud Ahmadinejad atatiliana sahii mikataba na serikali ya Sudani katika nyanja za uchumi, kukuza uhusiano wa kijeshi uliopo na wa kisiasa.
Iran ni moja ya nchi ambazo zinauhusiano wa karibu na serikali ya rais Omar Hassan al Bashir, ambapo serikali yake inapingwa na nchi za Ulaya Magharibi na Marekani kwa kuwekewa vikwazo vya kibiashara na kiuchumi.
Rais Al Bashir anaunga mkono sera ya Iran ya kuwa na mitambo ya kinyuklia, japo nchi za magahribi zinapinga kitendo hicho, kwa madai Iran inampango wa kutengeneza mabomu ya nyuklia.

1 comment:

Anonymous said...

may the GOOD LORD my find a better place for you MAMA AFRICA, R.I.P.