Thursday, September 22, 2011

Waizrael na Wapalestina watakiwa kukubalina ili kufikia muafaka wa amani

Waizrael na Wapalestina watakiwa kukubaliana ili kufikia muafaka wa amani.
New York
, Marekani - 21/09/2011. Rais wa Marekani amelihutubia balaza la umoja wa mataifa ya kuwa mgogoro kati ya Waizrael na Wapalestina utamalizwa kwa makubaliano yao wenyewe.
Baraka Obama alisema " Mgogoro uliyopo kati ya Waizrael na Wapalestina hunahitaji makubaliano ya pande zote mbili, hivyo lazima yawepo mazungumzo ili kuleta amani"
" Na uhusiano wa Amerika na Izrael hautatikishwa kamwe na haswa katika swala la ulinzi na usalama wa Izrael." Aliongezea Obama.
" Wapalestina wanatakiwa kuwa na taifa lao, na ndiyo maana Marekani imekuwa itoa misaada ya kuwasaidia Wapalestina ili kujenga taifa lao."
Hotuba ya rais Obama, imetangulia kabla ya rais wa Wapalestina Mohmoud Abbas ajatangaza ombi la wa Wapalestina kutaka kuwa wanachama wa Umoja wa Mataifa na kutambulika kama taifa hapo siku ya Ijumaa wiki hii.
Hata hivyo serikali ya Marekani imesema " itapinga kitendo cha Wapalestina kutaka kuwa taifa ikiwa ombi ilo litawakilishwa kwenye baraza la usalama la umoja wa mataifa."
Mgogoro wa Waizrael na Wapalestina umekuwa wa muda mrefu na wakuleta vichwa kuumu kwa jumiya ya kimataifa.

No comments: